Wema Sepetu: Hata mimi Ningekuwa Aunty Ezekiel Ningegombana na Wewe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Oscar ndauka
LICHA ya kupatana, habari ya mjini kwa sasa ni ugomvi mkali, wenye visa  vya kushangaza kati ya mastaa wawili wa sinema za Bongo, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel.Hii ‘kapo’ siku za karibuni, ilikuwa nzuri kwa maana ya urafiki wao mkubwa.Urafiki wa Wema na Aunt ulianza pale Wema alipoutengua urafiki wake na staa mwingine wa fani hiyo, Kajala Masanja.

Kuna visa lukuki kuhusu chanzo cha ugomvi wa Wema na Kajala, lakini ‘kuchukuliana’ bwana ndiyo kulitajwa sana!
Ikumbukwe kuwa, Kajala naye alirithi kijiti cha urafiki kwa Wema kutoka kwa msanii wa filamu na Mbongo Fleva, Snura Mushi.

TUREJEE KWA AUNT
Katika urafiki ambao ulionekana ungedumu zaidi ni kati ya Wema na Aunt kwa vile, Aunt alionekana kama mkomavu wa mambo ya ukaribu kuliko wengine, Snura na Kajala.Sasa siku za hivi karibuni, Magazeti Pendwa ya Global Publishers (ambayo huwa ya kwanza kufichua mambo ya siri ya mastaa), yaliandika kuhusu uhasama ulioibuka kati ya wawili hao chanzo kikiwa ni mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Mpenzi wa sasa wa Diamond, Zarinah Hassan ‘Zari’ aliandaa shoo aliyoiita Zari All White Party iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar.

UGOMVI ULIANZA KWENYE PROMO
Inajulikana kwamba, mtu anapoandaa shoo, kikubwa ni kuipigia ‘debe’ kwa maana ya kwamba, watu wajue kuna shoo kubwa ili waweze kuhudhuria kwa wingi na ndiyo mafanikio ya mwenye kuandaa! Wakati shoo hiyo ikipigiwa debe na vyombo mbalimbali vya habari sambamba na wadhamini, Aunt aliandika ujumbe wa kuisifia, kwamba itakuwa ya nguvu na si ya kukosa, akaitupia kwenye mtandao wake wa Instagram.

AUNT MNAFIKI?
Habari zilimfikia Wema kwamba, Aunt ametupia kwenye ukurasa wake akiisifia shoo ya Zari All White. Hapo ndipo pakawa pabaya kwa Wema akitafsiri kwamba, kitendo hicho kwake ni kibaya kwa sababu Zari yupo na Diamond ambaye yeye alikuwa mpenzi wake zamani, akammwaga! Tena hapa ieleweke sawa, Wema ndiye aliyemmwaga Diamond.

Kumbe Wema anaishi na kinyongo cha Zari kwa sababu amemchukua ‘wa zamani’ wake, Diamond. Kwa hiyo ana bifu! Akitokea mtu akampa 5 Zari, kwa Wema mtu huyo anakuwa adui kama ilivyokuwa kwa Aunt Ezekiel ambaye ameonekana ni mnafiki! Anachekaje na Zari wakati Zari na yeye ni maadui?! (eti).

KWA NINI AUNT ALIFANYA VILE LAKINI?
Aunt alikuwa na kila sababu ya kuifagilia shoo ile kwa sababu moja kubwa sana! Ameshamwanika mpenzi wake wa sasa kwamba anaitwa Moses Iyobo! Huyu dogo ni dansa kwenye kundi la Diamond. Kwa hiyo shoo za Zari ilitegemea sana madansa wa Diamond.

Hivyo, Aunt alitumia nafasi hiyo kuwataka watu wafike kwa wingi, ukumbi ujae kutokana na kiingilio na waonesha shoo, akiwemo Iyobo walipwe vizuri, ili maisha yake na Aunt ambaye kwa sasa ni mjamzito, yaendelee. Sasa Wema alitakaje? Aunt aseme; ‘msiende shoo ya Zari, itakuwa mbaya sana’! Halafu ‘mzee’ (Iyobo) aende kula za uso? Ni akili kweli?

HUU NI UTOTO!
Mimi nauona huu ni utoto uliopitiliza! Katika hilo la Wema kumwona Aunt ni msaliti au mnafiki, hata mimi kama ningekuwa Aunt ningegombana na Wema na wala moyoni nisingeona nimepoteza chochote!

AUNT NA IYOBO
Naamini Aunt na Iyobo bado wapo sana kimaisha kuliko Aunt na Wema. Mbaya zaidi ukizingatia Wema mwenyewe kila rafiki anayempata anampoteza kwa uadui! Maana yake nini sasa!

Mimi namshauri (Wema) akae chini na kutafakari kwa mapana mwenyewe, na si kwa kushauriwa na akina Petit Man au Martin Kadinda, ajiulize ni kwa nini yeye! Na si kujiuliza ni kwa nini marafiki zake wengi humaliza nao vibaya!
Anaweza kuamini ana nuksi kumbe si nuksi bali ni maisha ya ubinafsi! Cha kwake anataka akiendeshe yeye na cha wenzake pia anataka akiendeshe yeye, hayo si maisha Wema bwana! Chenji!

Source:Global Publishers
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. jingaz kabisa mtoa mada watu washapatana bado unajadili nini haswaa mnapendaaaaa kukuza mambo za watu nyinyi ni watu hamtawahi patanisha waliokosana daima dawamu! laitani ungejua apatae fadhila kwenye kupatanisha waliofarakana usingepoteza nguvu zako za vidole kuandika yaso na umuhimu mmeuzika eeehh???/ hamtauza juu ya kupatana kwao ndio wachimbua mambo mfyuuuu

    ReplyDelete
  2. Kwann anaumia ilihali yeye ndo alimwaga Nasibu!!!!

    ReplyDelete
  3. Kwann anaumia ilihali yeye ndo alimwaga Nasibu!!!!

    ReplyDelete
  4. kweli watu wa udaku mnampenda wema kila mara wema wema si mumuache jamani

    ReplyDelete
  5. acha unafiki na wewe admin umelipwa nini kwa hiyo umeona Wema ni mkosaji sana na wewe unaemwambia Wema achange wewe umekamilika au umeandika2 coz unajifurahisha bora alivomwambia kuliko kuendelea kumchekea rafiki ambaye ni mnafiki kwani asipo piga promo hawezi pew pesa Adimi acha unafiki umeona kua blog haisomwi bila kumposti Wema kaaaaaaaaaaaaaaaa@ watu wameshapatana bado mnarudia ujinga mnapenda kuona wenzenu wanagombana hafu nyie ndo mnafurahiiiiiiii fuuuuuuuuuuuuuuuyyyyyyyyyyyyyyyy

    ReplyDelete
  6. Kwani kuna mahali waliandika kuwa wamegombana au maneno ya washabiki.

    ReplyDelete

Top Post Ad