Sitta Awashangaa UKAWA...Awapa Jibu Hili Kuhusu Ahadi Wanazosema Watafanya Wakati Serekali Tayari inazifanya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri wa Uchukuzi, Samwel Sitta amesema serikali italifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATC) ili liweze kununua ndege nne na kuanza biashara.

Sitta pia amesema Rais Jakaya Kikwete atazindua ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha `standard gauge’ itakayogharimu Sh16 trilioni huku akiwataka viongozi wa vyama vya upinzani kuacha kuiba mipango ya serikali ya CCM.

Sitta amesema hayo leo alipokutana na waandishi wa habari jijini Dar ikiwa ni siku chache baada ya mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa wakati akifungua kampeni za chama hicho katika uwanja wa Jangwani, alisema akichaguliwa atajenga upya reli ya kati na kufufua ATC.

Waziri Sitta alisema anashangazwa na wapinzani kusema watajenga reli na kufufua ATC wakati hiyo ni ni mipango ya serikali ya CCM ambayo utekelezaji unaanza kabla ya uchaguzi.

Akifafanua, alisema Rais Kikwete Septemba 15 mwaka huu atazindua ujenzi wa reli katika eneo la Soga Mpiji wilayani Kisarawe na fedha hizo zitatoka katika benki ya Rolthschild ya Marekani.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad