Askofu Kilaini: Sifa kuu nne za mgombea ambaye atakuwa Rais wa nchi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Askofu wa kanisa Katoliki,
siku ya trh 26-09-2015 alinukuliwa akitaja sifa za mgombea anaepaswa kuchaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano Tanzania.

1. Mwadilifu
amesema nchi yetu ilipofika inahitaji mtu/rais ambaye anao uadilifu wa kweli na wa hali ya juu ili kuleta uongozi uliojaa uadilifu na nidhamu katika kuhakikisha kuwa watanzania wananufaika na kufurahia nchi yao na mambo yake yote.

2. Uchapa kazi kwa vitendo na Nidhamu,
nchi hii inayo rasilimali za kutosha ambapo zikitumika vyema watanzania watanufaika na maisha yao yatakuwa pazuri sana zaidi ya sasa hivi. Ili kuhakikisha hayo ni lazima tupate kiongozi mchapa kazikwa vitendo na hata tukimuuliza umefanya nini anao uwezo wa kutuambia nimefanya hili na lile.

3. Mtekeleza majukumu yake ipasavyo
kiongozi ambaye atakua Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania anapaswa kuwa ni mtekeleza majukumu anayopewa na yanayomhusu ipasanyo, kama umekabidhiwa jambo unalifanya kwa ukamilifu wake. Hivyo tanzania ya sasa haihitaji tena wajanjajanja ambao wanachekea watu huku hakuna utekelezaji wa majukumu yao ipasavyo.

4. Mzalendo
hakuna maendeleo tuyatakayo hapa nchini kwasababu viongozi wetu wengi sio wazalendo wa kweli, wanayoyasema hawayaishi, wanayoyahidi hawayatekelezi kisawasawa.

Hivyo basi 2015-2020 inahitaji wazalendo wa kweli na naamini mpaka sasa tumeona nani mzalendo anayezungumza kwa ukali na umakini kuwa atawasaidia watanzania na atapambana na ufusadi, wezi na kushughulika na wabadhilifu wa mali na uchumu wa nchi.

5.Mcha Mungu
katika utumishi uliotukuka na katika utumishi uliojaa haki na utawala makini na bora ni lazima tupate rais ambaye anayo hofu ya Mungu na nimcha Mungu kabisa. Mwaka huu watu wanaoigiza kuwa niwacha Mungu wanapaswa kukataliwa kabisa.Tuwachague watu wanaoonekana kuwa na hofu ya Mungu.

6.Mpenda watu
kupendwa na watu pia ni sifa muhimu sana, ila uwe unapendwa sio kwasababu unawapa rushwa, sio kwasababu uliwaandaa muda mrefu wakupende, sio wakupende kwasababu umewafanya watamani kumkomesha mtu au chama fulani. Iwe wanakupenda kwasababu ni mtendaji wa kazi, kwasababu unachukiwa wezi mafisadi, uwe wanakupenda kwasababu hupendi mchezo ktk kazi, iwe wanakupenda kwasababu ya uzalendo wako. Nawe pia uwe unawapenda kwasababu unayapenda maelendeleo yao na uwe unawapenda kwa kuwatendea kazi ipasavyo na sio kuwaibia mali zao.

7. Asiwe boss kwa wananchi
rais ajaye hapaswi kuwa boss/ meneja wa wananchi wake. Hii ni tabia chafu kwa rais kuwa au kujifanya boss au meneja wa taifa zima. Bali rais anapaswa awe mtumishi wa watu, achukue muda wake mwingi kuwazungukia wananchi katika maeneo yao kukagua shughuli za maendeleo na kushiriki pia, hivyo lazima uwe mkakamavu wa mwili na akili.

8.Ujasiri wa kuwakemea wasio waadilifu
rais wa tanzania 2015-2020 anapaswa kwa nguvu zote awe mjsiri wa kukemea na kuwaonya hata kuwachukulia hatua viongozi na watanzania wasio waadilifu. Ni lazma afanye hivyo kwa lengo la kujenga nchi yetu katika hali ya uadilifu ili kuimarisha umoja,mshikamano, ushirikiano hata usawa na haki. Tayari mmeshaona kiongozi mwenye ujasiri wa kufanya hivyo, na hata anayekerwa na wasio waadilifu.

Kwa kuzingatia hayo tutakuwa tumepata kiongozi chaguo la Mungu 2015-2020

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Toa kwanza boriti ktk jicho lako kabla ya kuangalia la kwako je yeye ni muadilifu? Atueleze sadaka kutoka Escorw kwa nini iingie kwenye account yake binafis na cio kanisa?

    ReplyDelete
  2. nawaonea huruma wachungaji wanaoshabikia siasa ivi watakuja kujibu ninin kwa Mungu hawa.

    ReplyDelete
  3. Hahahaaaaaa! mtachonga sana mwaka huu watu wa ukawa kwan kwa sifa hapo juu Ndgu yenu hakuna hata moja inayomtetea maan si muadilifu but Jembe la kazi kama kawaida ndani ya point zoteeee! Tupewe nin watanzania kama si Magufuli kwan ni Mkombozi wa rasilimali za nchi hii kumbukeni Tanzania ya sas inahtaji kiongozi kama Magufuli. Usikurupuke tu kutaka mabadiliko bila mpangilio wowte ule kwan viongozi wa mabadiliko hawapo kwenye chama pinzani tofauti na unafiki tu na kutaka ulaji tuuu! Hapa kazi tu mtajijua wenyewe, magufuli juuuuuu! mmi siangalii chama bali naangalia mtu wa kazi.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe mbumbumbu kweli,umesahau pesa za escrow alipewa milioni 80 TZS.yeye mwenyewe anaongea kitu ambacho hana hata sifa moja.Pili Hiyo kazi tu ipi,barabara zinaviraka,mbovu.Pili Hatutaki mabadiliko ya mtu ,hayatasaidia.Mabadiliko ya mfumo mzima.

      Delete

Top Post Ad