Mchepuko Unapokuachia Kumbukumbu Isiyofutika Maishani Mwako

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kuna michepuko mingine inaacha memories ambayo haifutiki na hutosahau maisha yako yote. Sijui kama ilishakutokea? Hata ukiwa na njia kuu yako na ukaachana na mchepuko, basi utakuwa na njia kuu yako kimwili ila kiakili na kiroho uko kwa mchepuko.Mimi hicho kitu kinanisumbua sana.

Nakumbuka ilikuwa mwaka 2007 nilipoajiriwa kwenye taasisi fulani, nikiwa na miezi minne tuu kazini na ugeni wangu, kuna siku tulikuwa na workshop training ya mambo ya IT. Tukakaa kila mtu kwenye computer yake kwa ajili ya training.

Baada ya lunch tukisubiri session ya mchana, nikawa nasoma emails na kucheki news kwenye mitandao mbali mbali. Akapita dada mmoja basi macho hayana pazia akaona nasoma email fulani (hizi za kufowadiana). Akaniambia email nzuri hiyo, nifowadie, akanipa email add yake. Nikafanya hivyo.

Kuanzia siku hiyo akawa ananirushia emails nyingi tu za kufowadiana, nikawa sina time nazo sana. Akawa ananitumia za kwake, ananisalimia na story nyingine nikaona kawaida. Sikushtuka.

Siku moja nikakuta amenitumia email, heading inasema "Nyumba hii unaweza kuipangisha kwa bei gani?" Nilipofungua nikakuta attachment ya slides, ina picha ya nyumba, kuna arrows kila chumba nikiclick inafunguka humo kuna picha za xx watu wanachapana, kila chumba.

Daah, nilipanic, ukweli nilikuwa sijawahi kuchepuka na nilikuwa mshamba mshamba wa hayo mambo, hata picha za x nilikuwa sipendi kabisa kuangalia. Ila siku hiyo nilipanic sana, mwili wote ukasisimka, mashine ikasimama nikiwa ofisini nikashindwa la kufanya. Siku nzima nikawa na mawazo, usiku niko kitandani namuwaza yule dada, nilikuwa na maswali mengi.

Siku iliyofuata akanipigia simu, nikashtuka amepataje namba yangu (anyway, labda kachukua kwa mtu mwingine, sikuhoji). Kuanzia pale mwanamume nikawa nimeshaingia ndani ya 18 yake. Alinisumbua sana, kwa siku alikuwa ananipigia tunaweza kuongea hata saa nzima au masaa mawili.

Ilipofika ishu ya mechi, alinipigisha kwata styles zote, mpaka zingine nilikuwa sizijui na ushamba wangu ujanani sikuwa na hayo mambo, sikuwahi kufanya sex mpaka siku ya ndoa. In short sikuwa na uzoefu.

Kilichonisaidia ni kuwa nilikuwa very strong kupiga round tatu au nne ilikuwa kawaida kabisa, na ikitokea tunaspend usiku wote basi mpaka tano. Mtoto anakata kiuno kama feni, ana miguno ya makelele, ananyonya mpaka unachanganyikiwa aisee. Kitu kimoja nilichokuwa naogopa, alikuwa mke wa mtu. Msiniulize ngoma tulienda kupima kabla ya kukutana.

Siku moja nikamwambia hatuwezi kuendelea hivi, mke wa mtu sumu. Akanijibu, sawa mke wa mtu sumu lakini haiui panya. Tukahitilafiana, akalia sana siku hiyo. Nikambembeleza aache kulia its over. Nikamhoji aniambie kwa nini amefanya vile, akatoka akaenda kwenye gari lake akaniletea albam ya picha, akanionyesha picha ya mumewe.

Alinisimulia mengi. Moja, amepishana na mumewe miaka mingi kiumri kwa hiyo hawamatch hata inapokuja suala la hobby. Pili mumewe ni mtu wa safari sana, nyumbani anaonekana kwa nadra sana, zingatia mumewe ni mchaga mambo ya business kwa sana.

Akaniambia kuwa hafurahii tendo la ndoa kwa mumewe, huwa anampa tu kama kutimiza wajibu lakini haitoki moyoni. Mwisho, akaniambia nikimuacha bora afe kwa vyovyote vile hataweza kukosa penzi langu.

Kuna siku alisafiri kwenda Dar, akaenda Zanzibar kuchukua mizigo ya biashara, aliporudi akaniletea box la zawadi amelifunga kwenye mfuko wa malboro mkubwa. Akaniambia nisifungue mpaka nifike nyumbani. Tulipoachana mimi nikaenda zangu ofisini nikague kwanza nisije nikaleta soo home.

Kumbe alikuwa ameninunulia mashati manne mazuri sana, vitambaa vya suruali viwili, viatu pea mbili vizuri, saa, simu smart phone, seti mbili za bed cover (mashuka manne, pillow nne, matandiko mawili) ya bei kali sana na rangi nzuri sana.

Pia nikakuta boxer nne, na bukta nne za kwangu, underwear nne na skin tight mbili za mke wangu. Kuanzia hapo akawa ananimiliki ile mbaya, daah, alikuwa ananibembeleza, alinivuruga nikavurugika kisawasawa.

Akisikia tuu nina tatizo basi kama ni hela ananipa, mara kapiga simu. Ila alinipa heshima sana akaniambia namba yake nisevu kwa jina la dereva tax, alikuwa hataki kabisa mapenzi yetu yavuruge ndoa zetu, kila mara ananikumbusha kufuta sms.

Ila kuna wakati tukavurugana tena tukaachana japo kwa machozi sana na vitisho. Sasa hivi ameacha kazi na amepata kazi green pasture nzuri zaidi mkoa mwingine, ila bado ananipigia na kunikumbuka. Since then, nimeshindwa kabisa kumsahau, japo najaribu kudelete hiyo file imeshindikana.

Nikitofautiana na mke wangu huwa natoka nyumbani naenda kukaa sehemu tulivu, najikuta namwaza yeye kama faraja, nammpigia, alafu nikiongea naye najikuta nalia nashindwa kujizuia. Wakati mwingine nikilala usiku najikuita hisia zinanijia natokwa na chozi.

Hivi nifanyeje nisimkumbuke tena? Ubaya mwingine ni kuwa njia kuu yangu imejisahau sana, no care tangu apate kazi ya kuajiriwa, maisha yanaenda tu ili mradi. Laiti mwenzangu angekuwa anajali may be ningesahau habari ya huyu mchepuko.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad