Bunge Kuondoa Ajira za Kudumu Serikalini.....Kudumu Kwa Ajira Ya Mfanyakazi Kutategemea Juhudi Zake Kazini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litafanyia mabadiliko makubwa sheria za utumishi wa umma kwa kuondoa ajira za kudumu serikalini, ili kuwezesha mabadiliko yaliyokusudiwa na Rais Dk. John Magufuli.

Katika mabadiliko hayo, mfumo sasa wa ajira za serikali kuwa za kudumu utabadilishwa na badala yake, kudumu kwa ajira ya mfanyakazi kutategemea juhudi na bidii yake kazini, ili kuondoa uzembe uliodumu miaka nenda miaka rudi, katika sekta ya umma.

Akizungumza katika mahoajino binafsi na gazeti la  Raia Mwema, mjini Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, alisema baadhi ya sheria za kazi zinawafanya baadhi ya watumishi wa umma kuwa wazembe.

Kwa mfano katika serikali ya sasa mfanyakazi mzembe kabisa kabisa hata waziri kumfukuza kazi hawezi. Hata Katibu Mkuu hawezi mpaka afuate mlolongo mrefu na hatua nyingi sana, yaani kazi ni guarantee (uhakika) katika nchi yetu ni permanent and pensionable (ya kudumu na ina pensheni). Sheria za namna hiyo lazima ziondoke,” alisema Spika Ndugai .

Katika nchi ambazo zinaendelea kwa haraka moja ya jambo ambalo huna uhakika nalo ni ajira, ukifanya vizuri unayo ajira yako ukiboronga unaondoka saa hiyo hiyo na wakati huo huo, sasa sheria za namna hiyo ni lazima zibadilishwe ili watu wachape kazi. Wawe wakijua kabisa kwamba nipo kwa sababu nachapa kazi akileta uzembe kazini kwaheri,” aliongeza.

Aliongeza kuwa mabadiliko mengine ambayo Rais Magufuli atayaleta ni pamoja na ile sheria ya ununuzi na sheria nyingine ambazo ni za hovyo hovyo, zinazoifanya serikali isifanye vizuri. Kwa mujibu wa Ndugai, Bunge litahakikisha sheria hizo zibadilishwa haraka.

“Huo ndiyo ushirikiano wetu tutakaompa lakini pia tutachangia vizuri katika mipango na bajeti zinazokuja tutazitengeneza vizuri zaidi kwa kupunguza fedha zote za ulaji ulaji, hii ya kila mwaka mapazia, kuweka makochi, kuweka makapeti na kompyuta kila mwaka na ofisi ni zile zile watu wale wale, bajeti ilikuwa imejaa ununuzi wa magari vilainishi lazima tukate kote huko,” alisema.

Akizungumzia hatua hiyo, Rais wa Shirikisho la Vyama wa Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Gratian Mukoba, alisema hawezi kuunga mkono au kukataa hoja hiyo mpaka atakapoona hoja yenyewe na maelezo yake.

Kwa kawaida muswada wa sheria huanzia kwanza kwa wadau, wakituletea tutaona, siyo kila kitu ni kibaya, sheria zinapotungwa zinakuwa na sababu kwa nini zimetungwa. Unaweza ukawa na maelezo mazuri tukajadili utekelezaji wake, tutaamua,” alisema.

Alipoulizwa kuhusu mwenendo wa baadhi ya watumishi wa umma kufanya kazi kwa mazoea na kama sheria hiyo inaweza kutibu tatizo hilo, alikiri kuwepo kwa hali hiyo miongoni mwa watumishi wa umma lakini akatahadharisha kwamba tiba yake siyo kuondoa ajira za kudumu.

“Ziko sababu nyingi zinazosababisha baadhi ya wafanyakazi kuwa wazembe, siyo ajira ya kudumu peke yake. Kama kwenye nchi yenu mmeamua kubaguana kwa malipo, mmoja analipwa mara 30 ya mwingine, huyo anayelipwa kidogo hawezi kuwa na morali ya kazi, atanyong’onyea.

Yule anayepata mara 30 ataathiriwa utendaji wake na hawa wenye kidogo kwa sababu ni wengi, kwa sababu watajifanya (wanaolipwa kidogo) na serikali itajifanya inalipa lakini kumbe kinacholipwa hakitoshelezi chochote,” alisema Mukoba.

Aliogeza kwamba miaka ya 1970 na 1980 watu walikuwa na uhakika wa ajira za kudumu lakini walikuwa wanachapa kazi kwa bidii kwa kuwa kulikuwa na uwiano wa haki kwenye malipo ya mishahara, tofauti na sasa, akishauri pia suala la kushuka kwa morali ya kazi miongoni mwa watumishi wa umma lifanyiwe utafiti makini na si kulikurupukia.

Chanzo: Raia Mwema
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. HIKI SASA NI KIAMA!!!!

    ReplyDelete
  2. Wewe ndungai usilete
    Tanzania kuna social system
    Mtu akiwa hana kazi atalipwa
    Cha msingi ni kuangalia hali ya maisha Na kipato cha wafanya kazi
    Pili sehemu zote zenye ulaji ni watoto na ndugu wa vigogo WA CCM

    ReplyDelete

Top Post Ad