Uwezi Amini Rais Magufuli Awa Gumzo Kubwa Nchini Kenya...Watamani Awe Rais Wao...Wamkosoa Uhuru Kenyatta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Uchapakazi wa Rais Dkt John Magufuli unatuma ujumbe si kwa maafisa wa Tanzania pekee, bali na nchi za jirani pia na kuwaacha viongozi wa nchi hizo kwenye wakati mgumu.

Kenya ambayo imekuwa ikifuatilia siasa za Tanzania tangu wakati wa kampeni, imeonesha kupenda mbinu za Magufuli na wananchi wake wanatamani mtu kama yeye.

Kwa kipindi kifupi alichoingia madarakani, Magufuli amefanya mambo makubwa na wananchi wamependa.

Ziara yake ya kushtukiza kwenye hospitali ya Muhimbili ilifichua uovu mwingi na kupelekea kufutwa kwa bodi ya wakurugenzi wa hospitali hiyo na kumuondoa Kaimu Mkurugenzi wake, Dk Hussein Kidanto.

Ili kupunguza matumizi makubwa ya fedha za serikali kwaajili ya kugharamia safari za nje za viongozi wa nchi, Magufuli aliamua kuzisitisha mara moja.

Dkt Magufuli pia alielekeza kiasi cha shilingi milioni 225 zilichangwa kwaajili ya kugharamia hafla ya wabunge kupongezana mjini Dodoma zipelekwe kwenda kununua vitanda. Badala yake shilingi milioni 15 pekee zilitumika kwaajili ya sherehe hiyo.

Siku chache baadaye vitanda hivyo na vifaa vingine vilinunuliwa na kupelekwa Muhimbili.

Jumatatu hii Magufuli alitangaza kuondoa sherehe za maadhimisho ya siku ya Uhuru December 9 na fedha za maandalizi hayo zitumike kwa mambo mengine muhimu.

Hayo na mambo mengine yamefanya Dkt Magufuli atrend nchini Kenya.

Hizi ni baadhi ya tweets za wakenya:
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

9 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kutupa kiongozi ambaye ana hofu ya Mungu,
    Tumuombee.

    ReplyDelete
  2. Mungu ampe nguvu baba huyu.
    kaka na dada zangu hawajawahi kupata mkopo wa elimu ya juu pamoja na kuwa na vigezo vyote,mimi leo nimepata mkopo,asante kutujali.Mungu ambariki.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Amina.Na sidhani kama wote wamepata mikopo ila anajaribu kubana kila idara ili mradi wenye kuhitaji mikopo wapate,Na trust me rais angekuwa Lowasa mkopo musingepeta kwa kisingizio hazina hakuna hela.Mungu amlinde daima.

      Delete
  3. EWE MWENYEZI-MUNGU TUNAKUOMBA UMLINDE NA UMPE UMRI MREFU RAIS WETU JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, INSHALLAH......AMEN

    ReplyDelete
  4. Mungu hujibu kwa muda unaofaa na kwa njia anayojua yeye,ila kamwe huwa hadharau maombi ya binadamu,uombe usiku ,mchana na mahali popote.
    Watanzania kwa muda mrefu tumelia tupate rais anaefanana na Nyerere,na sasa Mungu kajibu.Hakika anayembeza Magufuli kwa kasi hii aliyoanza nayo ni mvurugaji.ASANTE MUNGU.

    ReplyDelete
  5. Dear Man G Darkstar, hao CCM unao-wazungumzia kwamba ndio walosababisha uchumi kudorora, ni huyo Lowasa na kundi lake lote wamekimbilia katika 'kichaka' cha ukawa, walobaki CCM wote 'wasafi'........HAPA KAZI TU

    ReplyDelete
    Replies
    1. Eti wote wasafi?tushukuru mungu tumapata raisi mzuri na aendelee hivyo kwa miaka mingine,lakini kusema wote ccm wasafi huo ni ushabiki wako wa kisiasa na kampeni zimeisha,chenge msafi?

      Delete
    2. tibaijuka, muhongo, na wengine escrow na epa na safari zilizopindukia, makaa ya mawe kiwira kajimilikisha, gesi kupelekwa china, wakubwakutibiwa nje, watoto wao kusoma ulaya, dawa za klevya njenje, watoto wa vigogo kulisishwa shamba la bibi n.k

      Delete
  6. Mungu wet tunakushukuru sana juu ya rais wetu Magufuli. tunakuomba umlinde, umpe uhai, afya, nguvu, busara, uwezo zaidi na awe na maamuzi makini katika kila analolifanya kwa manufaa ya nchi hii na vizazi vijavyo. Tunaomba baba ifike mahali kila mtanzania aelewe kusudi uliloliweka ndani ya Magufuli ili wote tujue na kuelewa kuwa kazi ya halali ndio itakayotuondoa katika hali duni kwenda katika hali nzuri zaidi huku kila mmoja wetu akinufaika na rasilimali ulizotupatia katika nchi yetu. Mungu wetu tunaomba umfunike Magufuli kwa mikono yako asidhurike kwa chochote kile na zaidi umjaze hofu yako ile atende haki yako katika nyanja zote. Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania na watu wake, Mungu Mbariki rais wetu Dr JPMagufuli, AMEN

    ReplyDelete

Top Post Ad