WEMA Sepetu na Kajala Acheni Utoto..Maisha Yenu Tunayajua A-Z, Tengenezeni Pesa Kupitia Sanaa Zenu na si Kuhongwa na Kuja Kututambishia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wema Sepetu
KWENU warembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ na Kajala Masanja. Habari zenu binafsi? Bila shaka ni wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku. Kitambo kidogo sijawaona lakini naamini pumzi ya bure mnaendelea kuivuta ndiyo maana nasikia matukio yenu kwenye vyombo vya habari.

Mkitaka kujua afya yangu, mimi ni mzima. Namshukuru Mungu naendelea na shughuli zangu kama kawaida. Mungu ni mwema sana, anaendelea kubariki kazi ya mikono yangu, namuomba yeye aendelee kunibariki zaidi na zaidi.

Dhumuni la kuwaandikia barua hii ni kutaka kuwakumbusha kwamba nyinyi kwa sasa ni watu wazima. Umri wenu unatosha kabisa kusema haufanani na yale matukio yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Mara kadhaa nimewahi kuwaambia, hata yale mashindano yenu ya kumwaga fedha ukumbini, nyakati hizi si zake.

Mambo ya kuibiana mabwana kama yalishatokea, itoshe sasa kusema ulikuwa ni ujana. Kwa kuwa ilitokea, hakuna namna zaidi ya kuyasahau na kuchapakazi. Soko lenu la filamu bado haliridhishi, lakini mnapaswa kukomaa ili angalau mtengeneze fedha kupitia kazi zenu na si kuhongwa.
Binafsi sikufurahishwa na tukio lenu la kukutana ukumbini na kuzinguana mbele ya kadamnasi lililoripotiwa wiki iliyopita na magazeti Pendwa. Lilikuwa tukio linaloonesha kwamba bado hamjakua kitu ambacho sitaki kukiamini.
Wema na Kajala

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali, huu siyo wakati wa nyinyi kuoneshana ubabe wa fedha. Kwamba eti kwa kuwa mwenzako kaenda kutunza msanii jukwaani, na wewe lazima utunze nyingi zaidi ili uonekane wewe ni zaidi.

Ndugu zangu, bahati nzuri maisha  yetu tunajuana. Kwa kiasi kikubwa natambua maisha ya wasanii wetu nchini hususan warembo. Wengi wenu hamtegemei sanaa kuendesha maisha yenu. Wengi mnategemea  mapedeshee au ‘mabwana’ kutamba mjini.
Niwashauri hizo fedha mnazozipata ni bora mngewekeza kwenye sanaa yenu. Mkajizatiti vizuri ili ziweze kuzaliana. Mnapigana ili iweje? Mnatambiana mbele za watu inawasaidia nini. Wenzenu wanapigana siku hizi wanaingiza fedha.

Nyinyi kazi yenu si ubondia. Kazi yenu ni uigizaji. Igizeni kwelikweli na Watanzania wawaunge mkono kwa kununua kazi zenu. Sanaa yenu ina changamoto nyingi, mnawezaje kuzishughulikia ikiwa hamna umoja.

Mtawezaje kutatua changamoto hizo ikiwa hamna upendo kati yenu? Si rahisi kutatua changamoto hizo wakati mna chuki. Ili mfanikiwe, mnahitaji kushirikiana. Shirikianeni ili muweze kuisogeza sanaa mbele, acheni vita ya kipuuzi mnayoendelea kuifanya.

Mkizingatia hayo niliyowaambia, hakika tutaona mabadiliko kwenu na sanaa kwa ujumla. Nina imani nyinyi ni watu wazima na mtajipanga upya na mtaanza kuchapa kazi kama kauli mbiu ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli, ‘Hapa Kazi Tu’.

Ni mimi mtu wenu,
Erick Evarist.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

9 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwani kina nani hawa jamani
    Si malaya tu wauza sura tena zilizofubaa kwa kupikwa na hamira iliyo expire
    Kwa lipi
    Wangekuwa wazuri na shughuli wanaijuwa wangekuwa wake za watu

    ReplyDelete
  2. hata mke wa mtu naye ni malaya kama wewe Anony 12.11. PM

    ReplyDelete
  3. bora wao wauza sura wanapata wanachokitaka, jiulize wewe uamaliza mabaa yoote huna wa kukununulia chips.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kashfa kila kukicha
      Bongo si ughaibuni Malaya nyinyi
      Mtashindana na wasanii wa kike wa ughaibuni

      Delete
  4. My advise kwa wote wawili wakae wamalize tofauti zao ikiwa Mwenyezi Mungu humsamehe mja wake vipi wao washindwe wamlani shetani alie wasimamia dunia ni ndogo sana tujifunze kusameheana

    ReplyDelete
  5. ok na wewe erick evarist mtoa mada za kidada... umeshaandika maovu ya wenzio na wewe andika ya kwako tuyaone, usijifanye kutoa kibanzi kwenye jicho la mwenzio wakati jicho lako lina boriti. umeona ya kwako ya gizani sana hayaonekani.,, acha kufatilia maisha ya watu. fanya kazi za kiume. hapa kazi tu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. mapovu ya malaya utayajua tu

      Delete

Top Post Ad