Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo kuanzia jana.

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa ikimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imesema Rais amemteua Dk Charles Mlingwa ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Siha kujaza nafasi hiyo.

Mulongo anakuwa mkuu wa mkoa wa pili kutimuliwa kazi na Rais Magufuli baada ya Anne Kilango Malecela aliyekuwa Shinyanga.

Hata hivyo, tofauti na Kilango ambaye alitimuliwa kutokana na kutoa taarifa potofu kuhusu watumishi hewa mkoani mwake, Ikulu haikutoa sababu za kutenguliwa kwa uteuzi wa Mulongo.

Mulongo ameondolewa madarakani miezi sita baada ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Dk Faisal Issa baada ya kutofautiana na Mulongo wakati huo akiwa mkuu wa mkoa huo.

Baada ya kumwondoa Dk Issa na nafasi yake kujazwa na aliyekuwa Kamishna wa Polisi, Fedha na Utawala (CP) Clodwig Mtweve, miezi miwili baadaye Rais alimbadilisha Mulongo kituo cha kazi akimhamishia Mara.

Alipoulizwa jana jinsi alivyoipokea hatua hiyo iliyochukuliwa dhidi yake Mulongo alisema: “Sina taarifa rasmi.”

Kabla kuhamishiwa Mara akitokea Mwanza, Mulongo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Alishika nafasi hiyo baada ya kupandishwa cheo akiwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

5 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mwenzako akinyolewa - nawe jiandae huyu RC kiukweli alimufedhehesha swahiba wangu Dkt. Faisal Issa kwa ubabe usiokuwa na maana. Sasa iwapo kuachishwa kazi ni kuzuri ngoja kwa muda huu naye aonje kikombe hicho

    ReplyDelete
  2. Waandishi naomba kutoa
    Hoja kuna tofauti gani ya kutengua na kufanya mabadiliko ya viongozi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Yeh ! useme wewe kiazi , nikisema mimi Muhogo naambiwa nina mizizi ,
      humu kiswahili kibovu sana , halafu wanawacheka Wakenya
      Wakati mmoja ....niliona Superwoman wa Wanawake ...Rejea taarifa ya Joyce Kiria hapo kando
      Wakati mwingine hufikiria hawakwenda shule ya Uwandishi au Lugha inawapiga chenga .....
      Hawaelewi hawajitambui , hata kutengua na kufanya mabadiliko hawakujui
      Ahsante Anony 10.09 AM

      Delete
  3. HOJA IMEPITA NA IMEUNGWA MKONO

    ReplyDelete
  4. Kutenguliwa ni sawa kufukuzwa kazi?
    Au anabakia kwenye ajira mshahara wa bure hadi upangiwe kazi nyingine ?

    Bana matumuzi hiyo

    ReplyDelete

Top Post Ad