Wema Sepetu na Idris Sultam Wamwagana Rasmi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

DAR ES SALAAM: Ubuyu wa motomoto wa mjini ni kwamba, zile mbwembwe zote za penzi la mastaa wawili Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Idris Sultan, zinadaiwa kufikia ukingoni na sasa imebaki stori kwani Wema, Idris wamwagana rasmi.

Wikienda limeng’atwa sikio kuwa, kitendo cha wawili hao ‘kushoo lavu’ kwenye ile Pati ya Black Tie iliyofanyika juzikati katika Ukumbi wa King Solomoni pale Namanga, Dar ilikuwa ni geresha tupu kwani walishamwagana kitambo.

Hata hivyo, kama utakumbuka au hukuipata ni kwamba iliwahi kuvujishwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wema na Idris wamemwagana lakini baadaye zilivunjwa picha zikiwaonesha wakiwa wameshikana mikono na mahaba tele ili kuua soo.

wema-na-idriss-insta Sasa ubuyu ulionyooka kutoka kwa chanzo cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao unadai kwamba, kilichotokea kwenye pati hiyo zilikuwa ni mbwembe za kuzuga zilizotokana na huruma ya Idris.

Ilidaiwa kwamba, Idris alilazimika kufika kwenye sherehe hiyo kwa sababu ilishatangazwa kuwa atakuwa ni miongoni mwa ‘ma-hosti’ lakini ukweli ni kwamba mambo yalishaharibika.

wema na idris 2“Unajua watu wengi hawakujua kuwa Wema na Idris walishaachana kitambo na pale (King Solomoni) walikuwa wanafanya maigizo tu, japokuwa haijulikani moja kwa moja sababu ya kuachana kwao lakini Wema anadaiwa kuwa tatizo kwa Idris kutokana na kutokea kwa migogoro ya kila kukicha,” alitonya sosi huyo.

Hata hivyo, katika kuonesha kwamba kuna kitu kinaendelea, wana-ubuyu wetu walifuatilia akaunti zote za mastaa hao katika mitandao ya kijamii kuona kama mbwembwe zao zinaendelea na kubaini kuwa hawako sawa baada ya kusoma ujumbe wa Wema unaoonesha kumbembeleza Idris huku jamaa huyo akionesha wazi kuwa hakuna mapenzi bali ni drama tu.

Ili kuleta ushahidi, tunakukaribisha hapa kusoma nukuu zao mtandaoni;

MANENO YA WEMA
“Having you as a friend, a brother, a lover and of course a shoulder to cry on every time, i’m at my worst has been the best feeling ever… I wouldn’t want to lose this feeling over anything…
“I realized without u then i ain’t complete…. You have stood by me in good times and bad and even when i messed up so bad you would look me in the eyes and tell me, “Baby, its okay, we gona fix this”…
“Idris you have been one of a kind and losing u is the last thing i want on this earth… I will love you until forever, until death do us part we will be together…
“I will hold on to you till da last minute because together we will get there…. I love you with my life…. For I believe you are my true love, my baby and inshallah! The Man that my kids will call daddy…” alimalizia kuandika Wema akimlilia Idris.

IDRIS NAYE ALIANDIKA:
“Kumbuka kurekebisha kiatu kila hatua ya maisha unayopiga kisije kuchomoka ukakanyaga mwiba ukapunguza spidi.”

WEMA ASAKWA
Wikienda halikuishia hapo kwani lilimsaka Wema anayedaiwa kubwagwa, alipopigiwa simu hakupokea, akaandikiwa ujumbe mfupi wa sms ambao pia hakuujibu.
Pia alitumiwa ujumbe kwa njia ya WhatsApp lakini pia hakujibu.

 UBUYU WAKAMILIKA KWA IDRIS MWENYEWE
Wikienda liligeuza dira yake na kuielekeza kwa Idris ambaye alifunguka bila kuacha lolote.
Kwa mujibu wa Idris, yeye na Wema walishasahau kuwa waliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kwani kwa sasa kila mtu ana ‘biashara’ zake.

“Mimi nilikwenda kwenye ile pati kwa sababu ya kuwaonea huruma tu kwani ndiyo kwanza wameanzisha kampuni na mbaya zaidi walikuwa wakiniweka kwenye matangazo. Unadhani watu wangewachukuliaje? Sikutaka kuwaharibia shoo lakini mimi nilishaachana naye na nina biashara zangu nyingine,” alifunguka Idris.

Idris alienda mbali zaidi na kusema kuwa kwa sasa ana mwanamke mwingine anayempenda na siku si nyingi mambo yakikaa sawa, atamuanika.
“Mwenzenu nina kifaa kingine soon nitawafahamisha,” alisema Idris.

WEMA NA IDRIS
Awali Wema na Idris walificha uhusiano wao lakini baadaye waliamua kujiachia ambapo mlimbwende huyo alidai kushika ujauzito lakini kwa bahati mbaya ukachoropoka.

Source:Global Publishers
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. siaamini Kiki siku hizi ziko za aina nyingi sana.

    ReplyDelete
  2. Ngoja na mimi nijaribu bahati yangu kwa Wema,Kisha nionje halafu nasepa zangu.

    ReplyDelete
  3. pole sana mamitooo

    ReplyDelete

Top Post Ad