Diamond Platnumz Anunua Rolls Royce ya $400,000 na zaidi?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Huenda Diamond Platnumz akawa ameitimiza ndoto aliyokuwa nayo kwa miaka mingi – kumiliki gari alipendalo zaidi, Rolls Royce.

Kwa muda mrefu, staa huyo amekuwa akisema kuwa hilo ndilo gari analotaka kulimiki kiasi cha kujipa jina ‘The Rolls Royce Musician From East Africa.’

Diamond ambaye yupo jijini Los Angeles, Marekani alikoenda kushoot video ya wimbo aliomshirikisha Ne-Yo, ameshare kipande cha video kwenye Instagram cha gari hilo na kuashiria kuwa huenda akawa amelinunua tayari.

Hata hivyo hajasema iwapo gari hilo limeshakuwa mali yake ama alikuwa tu showroom kuosha macho!

Rolls Royce, ni magari yanayozalishwa na kampuni ya Uingereza na yalianzishwa na Charles Stewart Rolls na Sir Frederick Henry Royce, March 1906. Bei yake huanzia $300,000 – $500,000.

“Nataka nibadilishe aina ya gari sababu imekuwa ni muda mrefu, nafikiri ni muda wa kuwa na gari nililokuwa nalitamani siku zote, gari la ndoto yangu ni Rolls royce na ndio ninalotaka kulinunua mwaka huu wa 2016 na litakuwa na jina la PLATNUMZ na sio namba za kawaida,” aliiambia tovuti ya Millard Ayo miezi kadhaa iliyopita.

Alidai kuwa kwa alipofikia ni muhimu kwa na gari la hadhi yake ili kujiongezea thamani zaidi.

“Ndio maana nikipata Rolls Royce inatengeneza heshima,” alisema.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

10 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Anunue ajambeer...

    ReplyDelete
  2. Huyu naye shoga Kama wema ?
    Inatuhusu nini sisi nunua hata ndege
    Usiiige mastaa wa USA na ulaya wewe
    Bado una tongotongo za macho
    Unaishi bongo wapenzi wako 99% hawajui kesho watakula nini?
    Unaleta hapa acha ushamba Domo wewe

    ReplyDelete
  3. unafikiri RollsRoyce ni makalio kila mtu anaweza kuwa nayo eeeeh.. Hyo $400000 unayoiongelea ni bei yake likiwa huko hadi uliendeshe hapa tz itakucost $ 600000 na hilo ni old lady ghost bado hajaongelea mashine kama ROLLSROYCE WRAITH bado hajafika huko

    ReplyDelete
  4. unafikiri RollsRoyce ni makalio kila mtu anaweza kuwa nayo eeeeh.. Hyo $400000 unayoiongelea ni bei yake likiwa huko hadi uliendeshe hapa tz itakucost $ 600000 na hilo ni old lady ghost bado hajaongelea mashine kama ROLLSROYCE WRAITH bado hajafika huko

    ReplyDelete
  5. WEWEWEEE MWANAWANE KAZA BUTI UTIMIZE NDOTO ZAKO!!!

    ReplyDelete
  6. Replies
    1. tena mapovu meng, kaza buti usirudi nyuma, kwani hizo $ 600,000 ni shs ngapi bhana??????

      Delete
    2. Kuna wewe alikja huku kiinglio dola 10
      Masta wa USA dola 100 na kundelea
      Labda anabeba kwani tuna sikia Naye punda

      Delete
    3. watu wanatoka povu.hawa ndo wengine hawana hata laki mfukoni afu bado wanaita wenzao maskini.yamewafika hapaaaaaaaa.nyie ndo wachawi msiopenda maendeleo ya mtu.hela c zake kama hauna ni wewe.endeleeni na fitina zenu hamtazuia chochote

      Delete
  7. The cars produced between 1971 and 1977 boast with 6.75-liter V8 engine, 3-speed automatic transmission, a solid and strong exterior and super luxury interior with leather and all kinds of other spoils.automoves

    ReplyDelete

Top Post Ad