Meneja wa Diamond Athibitisha Kuwa ni Kweli Diamond Kanunua Nyumba Afrika Kusini..Ataja Bei Aliyolipia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kuna nyumba ilikuwa sokoni inayofanana na ile Diamond amedai kuinunua South, zinafanana tu ama ni ile ile? Hilo ni swali ambalo hadi sasa wengi wamekuwa wakijiuliza, lakini sasa Bongo5 ina jibu la uhakika.

Wiki iliyopita Diamond Platnumz alitengeneza vichwa vya habari baada ya kupost kwenye Instagram picha ya nyumba anayodai ameinunua nchini Afrika Kusini itakayotumiwa na mchumba wake Zari.

Picha hiyo aliisindikiza na maelezo mazito yaliyowalenga wale aliowaelezea kama wanaopenda kujisifia ni matajiri na kumuita yeye maskini ilhali watoto wao bado wanaishi kwenye nyumba za kupanga. Wengi walitafsiri kuwa dongo hilo lilimlenga ex wa Zari, Ivan anayefahamika kwa kuishi maisha ya kifahari.

Hata hivyo, muda mfupi baada ya Diamond kuweka picha hiyo, wametokea watu ambao wamesambaza picha ya nyumba nyingine inayofanana kwa karibu asilimia 100 na nyumba ile iliyowekwa kwenye mtandao wa privateproperty.co.za na hivyo kuzusha minong’ono mingi.

Kwa mujibu wa meneja wa Diamond, Sallam, nyumba hiyo imelipiwa Alhamis iliyopita na tayari ni mali ya muimbaji huyo wa Salome na amefafanua kwanini bado haijatolewa kwenye tovuti hiyo.

“Nyumba imelipiwa thursday haiwezi toka muda huo huo kwenye website mpaka agency amalizane na mwenye nyumba then process zote zikamilike ndio inatolewa kwenye site,” Sallam ameiambia Bongo5.

Nyumba hiyo ipo Moreleta Park, mjini Pretoria.


Ina vyumba vitano, lounge 3, mabafu matatu, bwawa la kuogelea, balcony, gereji mbili na nyumba ya pembeni ya kuishi wafanyakazi.

Ipo kwenye eneo lenye ukubwa wa mita za mraba, 1068.


Bei yake si haba, ilikuwa inauzwa kwa Rand 2,480,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 396 za Kitanzania.

Kuhusu anachokisema Diamond baada ya watu kudhani kawapiga changa la macho watanzania, Sallam amejibu, “Anachukulia kawaida, ni mengi kila siku yanasemwa.”

Hiyo ni sababu kubwa staa huyo ameamua kujizawadia mapumziko mahsusi visiwani Zanzibar mwishoni mwa wiki.

UPDATES:

Kibao cha ‘SOLD’ kimeshaweka kwenye nyumba aliyonunua Diamond, Pretoria, Afrika Kusini na tayari imeshatolewa kwenye listings za mtandao wa http://www.privateproperty.co.za. Na sasa ni mali yao halali..


Source:Bongo5
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. sisi tulijua nyumba ina jina la zari,kumbe sivyo hivyo sasa kwann kasema kamnunulia zari??? maana ya madale alisema ni nyumba ya tifa kumbe sio kweli ni nyumba ya mama yake mzazi na iko kwenye jina la mama yake,,,haya leo kanunua nyumba yake south na iko kwenye jina lake halafu anasema kamnunulia zari na wakati sio kweliii'''yeye aseme tuu kanunua nyumba south sio kamnunulia zari hiyo ni changa la machoo tuu>>>kutaka kupata kiki amnunulie subutuuu labda mama dangote afe...kamwe haiwezekaniiii hataaaa...

    ReplyDelete
  2. sisi tulijua nyumba ina jina la zari,kumbe sivyo hivyo sasa kwann kasema kamnunulia zari??? maana ya madale alisema ni nyumba ya tifa kumbe sio kweli ni nyumba ya mama yake mzazi na iko kwenye jina la mama yake,,,haya leo kanunua nyumba yake south na iko kwenye jina lake halafu anasema kamnunulia zari na wakati sio kweliii'''yeye aseme tuu kanunua nyumba south sio kamnunulia zari hiyo ni changa la machoo tuu>>>kutaka kupata kiki amnunulie subutuuu labda mama dangote afe...kamwe haiwezekaniiii hataaaa...

    ReplyDelete
  3. Si bora kununua kimya kimya kwani lazima dunia nzima wajue kama amenunua nyumba.

    ReplyDelete

Top Post Ad