Mambo Yazidi Kuwa Magumu kwa Wadaiwa Bodi ya Mikopo, Sasa Kukatwa 15% ya Kipato Chao kwa Mwezi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MAMBO yanazidi kuwa magumu kwa wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu baada ya asilimia ya marejesho ya mkopo huo kwa kila mwezi kuongezeka kutoka 8% hadi 15%.

Mabadiliko haya yamekuja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kuwa tayari amekwishasaini mabadiliko ya sheria yanayomtaka mwajiri kukata asilimia 15 ya mshahara wa mwajiriwa ambaye ni mnufaika wa mkopo wa elimu ya juu kwa ajili ya kulipa deni lake analodaiwa na Bodi ya Mikopo.


Hatua hii imekuja ikiwa wadaiwa hao tayari wamepewa siku 30 na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Abdul Razaq, aliyesema wadaiwa hao sugu watachukuliwa hatua kali iwapo hawatarejesha mikopo hiyo ndani ya mwezi mmoja.

Katika maelezo yaliyotolewa jana na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya, wakati akijibu maswali ya wananchi kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachoendeshwa kupitia mtandao wa facebook wa East Africa Television, Naibu Waziri Manyanya alisema sheria hiyo tayari imesainiwa na siku za hivi karibuni itaanza kutumika.

“Hii asilimia 15, kimsingi ninavyofahamu ilishasainiwa, baada ya hapo kuna kuiangalia iendane na kanuni zetu, baada ya kuicheki imeendana na kanuni zetu kama kuna sehemu itahitaji kuboreshwa kidogo haitazidi miezi miwili au mitatu, baada ya hapo tutaweza kutumia hiyo 15%, na asilimia 15 ya safari hii ni tofauti na siku za nyuma, siku za nyuma tulikuwa tunachaji asilimia 8”, alisema Manyanya.

Hapo awali wadaiwa hao wa mikopo walikuwa wanakatwa asilimia 8, lakini sheria ya sasa itaruhusu wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu kukatwa asilimia 15 ya kipato chao.

Pia Manyanya amesisitiza kuwa kwa wale ambao hawajaajiriwa, lakini wanafanya biashara zao wanatakiwa kuwasilisha angalau shilingi 120,000 kila mwezi na kuwashauri kuwa ni vema wakapeleka zaidi ili wamalize haraka madeni yao.

Kuhusu wasio na kazi, amesema haiwezekani mtu asome halafu akose shughuli ya kufanya na kuwataka kutafuta shughuli yoyote ya kufanya ili waanze mapema kulipa madeni yao ndani ya miaka miwili baada ya kuhitimu masomo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad