Huu Ndio Upasuaji wa kurudisha Bikra Kwa Mwanamke Unavyofanywa ..!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


bikra ni nini?

hii ni ngozi laini sana inayofunika uke kwa wanawake ambao hawajawahi kushiriki ngono kabisa, kikawaida mwanamke anaacha kuitwa bikra pale ngozi hii inapoondolewa.... ngozi hii kitaaamu inaitwa hymen.

hymenorrhaphy ni nini?

huu ni upasuaji unaofanyika kuirudisha bikra ya mwanamke ambayo imeshatoka tayari kwa sababu mbalimbali.

aina hii ya upasuaji mara nyingi hazipatikani kweye hospitali za kawaida kwani hazina umuhimu wowote kwenye matibabu na zinaweka kwenye kikundi cha plastic au cosmetic surgery,hivyo mara nyingi hufanyika kwenye hospitali au clinic binafsi na mabingwa wa magonjwa ya akina mama yaani gynacologist..

idadi ya wanawake wanaofanyiwa aina hizi za upasuaji inazidi kuongezeka miaka inavyozidi kwenda mbele kutokana na watu kuanza ngono mapema sana.

watu gani wanatakiwa wafanyiwe aina hizi za upasuaji?

wanawake ambao wanataka kurudisha bikra zao ambazo zimeshatoka wanatakiwa kufanya upasuaji huu kwani hakuna dawa yeyote inayoweza kurudisha bikra na ukiisikia ujue ni utapeli.

katika hali ya kawaida bikra inaweza kutoka kwa kushiriki ngono, kupata ajali na kuumia, tabia ya kujichua, mazoezi kama kuendesha baiskeli au farasi, matumizi ya aina fulani za pedi  au magonjwa fulani fulani.

wakati mwingine ngozi ila ya bikra inaweza kua ngumu sana kiasi kwamba ikakataa kuchanika hata kwa kuingiliwa kingono. hivyo mwanamke kutotoka damu wakati wa ngono kwa mara ya kwanza haimaanishi kwamba mwanamke sio bikra.

kwanini wanawake wanafanya aina hizi za upasuaji?

wanawake hua wanasababu mbalimbali kama ifuatavyo

   1 kuwaonyesha wanaume zao au jamii zao kwamba wao ni mabikra kipindi cha ndoa hasa kwenye jamii fulani fulani ambazo bikra ni muhimu sana siku ya ndoa.

  2  kuwasaidia wenye maumivu ya kisaikolojia baada ya kubakwa, hii inawafanye wapate amani kidogo baada ya upasuaji huu.

   3 kurudisha bikra ambayo imeharibika sababu ya kuumia kwa ajari.

upasuaji huu unafanyikaje?

hii ni aina ya upasuaji mdogo ambayo inafanyika kwa kuchoma sindano ya ganzi tu na wala haihitaji kwanamke kupewa dawa za usingizi, japokua kuna wakati mwingine kutokana na mazingira ya mgonjwa daktari anaweza kulazimika kutoa dawa ya usingizi.

kuna aina tatu za upasuji za kurudisha bikra kama ifuatavyo.

  1  kuishona tena ngozi ile ya ya hymen ambayo inamfanya mwanamke aitwe bikra kwa kuirudisha pamoja na kuiacha ipone kisha kurudi kama zamani

  2  kuweka ngozi ya hymen ya bandia na kuishonea pale kisha kuweka ndani yake aina fulani ya kimiminika kinachofanana kabisa na damu ili damu ionekane ikitoka  wakati wa ngono

  3  kuikata ngozi ya hymen ambayo ilichanika mwanzoni na kuitoa nje kisha kuirudishia upya na kuishona kabisa kama mwanzo.

wanawake wanaofanya aina hii za upasuaji wanatakiwa wafahamu kwamba wanatakiwa wakae bila kushiriki ngono wiki tatu mpaka miezi mitatu ili bikra ishike vizuri hivyo ni vizuri kuifanya mapema kabla ya ndoa sio unataka ufanyiwe leo afu wiki ijayo uolewe.

nyuzi zinazotumika kushona ngozi ile ya bikra hua haziondolewi yaani baadae huyeyuka ndani kwa ndani.

madhara ya upasuaji huu

upasuaji huu ni salama kabisa ila hua una madhara madogo madogoambayo ni kawaida hata kwa uparesheni zingine kama ifuatavyo.

kutokwa damu; hii ni kawaida hata kwa uparesheni zingine lakini damu hii inatakiwa ikauke na kuondoka baada ya siku chache.

kubana sana; wakati mwingine daktari anaweza akaishona ngozi ile na kuibana sana kiasi kwamba ikawa ngumu sana siku ya kuitoa wakati wa kushiriki ngono. hua na maumivu makali ambayo huisha bila dawa yeyote baadae.

infection; hii husababishwa na kushambuliwa na bacteria baada ya upasuaji lakini huweza kuzuiliwa kwa kupewa dawa za kuzuia hali hii mfano antibiotics

mwisho; aina za upasuji hizi zinapatikana nje ya nchi kwa wingi, kwa nchini tanzania na afrika kwa ujumla zipo pia lakini ni sehemu chache sana.

dunia inakwenda kwa kasi sana hivyo mwanaume ukijikuta umeoa bikra mwenye watoto wanne usishangae...
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad