HELA Wanazotuhumiwa Kupewa Kina TID Zilitolewa na Nani na Kutoka Fungu Gani?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Clip iliyosambaa toka jana katika mitandaoni ya kijamii akisikika Mama Wema Sepetu na Steve Nyerere imezua Maswali mengi ikiwemo haya hapa chini:


1.Hiyo milioni mbili inayotajwa kuwa TID kapewa imetolewa na nani?

2.Kama kweli baadhi ya walionekana kwenye vyombo vya habari watakuwa wamepewa hela, itakuwa wamepewa jumla ya shilingi ngapi?

3.Inawezekana mtu akatoa hela hizo zote kutoka mfukuoni mwake?

4.Kama kuna kikundi au taasisi ndio imehusika kutoa hizo fedha,watatoa tu hela zao hivi hivi bila kuwa na maslahi?

5.Kama kuna maslahi,yatakuwa ni maslahi gani?

6.Kwasababu zoezi hili lilikuwa likiratibiwa na serikali,inawezekana kuna mkono wa serikali?

7.Kama kuna mkono wa serikali,ni afisa gani kahusika na amezitoa katika fungu gani?

8.Kama hizi "clip" ni fake,kuna yoyote miongoni mwa wanaotajwa amejitokeza kukana yanayosemwa?

9.Mama Sepetu na Steve Nyerere kuna yoyote kati yao amejitokeza kuzikana hizo clip mpaka sasa?

10.Kama hizi clip ni za kweli, Mama Sepetu na Steve Nyerere hawatashili kuhojiwa na vyombo husika?

11.Swala hili likipita pasipo wahusika kuhojiwa au likaishi tu kimya kimya,itakuwa ni hivi hivi tu?

12.Wote wanaotajwa kama kweli wanasingiziwa, ina maana wote mpaka muda huu wameshindwa kutumia hata mitandao ya kijamii kukanusha /kutolea ufafanuzi?

Kama kina TID walipewa/hawakupewa hizo hela basi tunaomba kina TID na hao wenzake wajitokeze hadharani wakanushe au wakiri kupewa hizo fedha lakini wakikiri watuambie walipewa na nani.

Mwisho kama ni taasisi ya serikali ikihusika bila shaka taratibu zilifuata hivyo tutaomba kuona document za malipo hayo.

Ukiona giza linazidi,ujue ndio kunakaribia kukucha.

By Salary Slip

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad