MAHAKAMA Yabariki Kuvunjika Kwa Ndoa ya Flora Mbasha na Mumewe...Sasa Kugawana Mali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Baada ya msuguano wa miezi kadhaa, hatimaye Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni imeridhia kuvunja ndoa ya Mwanamuziki wa Injili, Flora na mumewe Emmanuel Mbasha kisha kugawana mali walizochuma pamoja. Chanzo makini kimefunguka kuwa, Flora aliyekuwa akiidai talaka hiyo ili aweze kuolewa na mwanaume wake mpya, alifanikiwa azma yake hiyo hivi karibuni baada ya mahakama kuridhia.

“Si unajua Flora ameshapata bwana mpya yule Daud Kusekwa na vikao nasikia vimepamba moto. Hivyo alikuwa anapambana kwelikweli kuhakikisha anapewa talaka na mimi ninayo nakala yake kama vipi niwatumie.

“Sasa amefanikiwa, wamegawana mali na mahakama imewapa masharti juu ya malezi ya mtoto wao aitwaye Eliza kwamba Flora ndiye atakayempa mahitaji yote ya msingi,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Si unajua wale kuna mali walichuma pamoja? Basi zote wamezipiga pasu. Kuanzia zile zilizokuwa kwenya akaunti ya pamoja na hata ile nyumba yao iliyopo Tabata Kimanga.”

Risasi Jumamosi baada ya kuipata nakala ya hukumu hiyo ya talaka, lilimvutia waya Flora ili kumsikia anazungumziaje hatua hiyo lakini simu yake haikupatikana hewani.

Kwa upande wake Mbasha, alikiri ndoa yao kuvunjika mahakamani na kusema hayuko tayari kuzungumzia mgawanyo wa mali zao. “Wewe elewa tu tumeshaachana, talaka imetoka mahakamani.

Hayo mambo mengine mimi siwezi kuyazungumzia,” alisema Mbasha. Wawili hao kwa sasa kila mmoja ameshampata mwenzi. Flora anatarajia kuolewa Aprili 30, mwaka huu wakati Mbasha bado haijajulikana kama atamuoa mchumba wake wa sasa au la.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mmh jipe moyo leo imegeuka mkuki kwa mbasha

    ReplyDelete

Top Post Ad