Zitto Kabwe Aandika Ujumbee Huu Baada Ya Godbless Lema Kunyimwa Dhamana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyokaa Arusha kutupa Rufaa zote mbili zilizofunguliwa na Serikali dhidi ya maamuzi ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kuhusiana na dhamana ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amezungumza.

Kiongozi huyo wa ACT ametumia Facebook kutoa malalamiko yake:
Mnamkamata mtu kwa kosa lenye dhamana. Mahakama Kuu inaruhusu dhamana. Serikali inakataa rufaa kuzuia dhamana. Mtu anakaa jela miezi 4, tena mwakilishi wa watu. Siku ya hukumu kuhusu dhamana Serikali inaondoa shauri mbele ya jopo la majaji 3. Lengo? Kumkomoa mtu. Siasa za ukomoaji zinajenga chuki kwenye jamii na chuki inazaa visasi. Haitoshi majaji kukemea Ofisi ya DPP. Mfumo wetu lazima uweke uwezo wa waendesha mashtaka wa aina ya kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini kuwajibishwa. Wanasheria tazameni namna ya kuwajibisha ofisi ya DPP kwa uonevu wa makusudi dhidi ya wananchi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad