BABU Ambaka na Kumpatia Ujauzito Mjukuu Wake..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Polisi mkoani Mwanza inamshikilia mkazi wa mtaa wa Nyasaka wilayani Ilemela mwenye miaka 66 kwa kumbaka na kumpata ujauzito mjukuu wake mwenye umri wa miaka 16.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema tukio hilo liligundulika Aprili 25.

Alisema mwanamume huyo alikuwa akiishi na mjukuu wake  (jina linahifadhiwa) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Nyasaka.

“Mtuhumiwa alikuwa akiishi na mjukuu wake tangu mwaka 2011 akitokea Musoma vijijini na alikuwa akimfanyia ukatili wa kingono kwa kumwingilia kimwili wakati  mkewe hayupo,” alisema Msangi.

Kamanda huyo alisema mtuhumiwa alikuwa akimtisha kuwa atamwachisha shule na kumrudisha kijijini kwao mjukuu wake endapo atatoa siri kwa mkewe au ndugu zake.

Msangi alisema kutokana na vitisho hivyo, binti huyo aliendelea kuvumilia hali hiyo pasipo kumwambia mtu na Aprili 25 walimu walitilia shaka hali ya afya yake na alipopelekwa hospitali kupima iligundulika ana ujauzito wa miezi minne.

“Walimu walimhoji aliyempa ujauzito na alidai ni babu yake. Walitoa taarifa kituo cha polisi ambapo walifanya ufuatiliaji na kumkamata mtuhumiwa,” alisema Msangi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad