Hii Inaitwa Bampa Tu Bampa..Kiongozi wa Korea Kaskazini Amjibu Trump ..Awaandaa Makombandoo Wake Tishio Kuikabili Marekani..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


KIONGOZI wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un ameanika kikosi chake maalumu cha kijeshi kwa mara ya kwanza mwishoni mwa wiki hii, kama hatua ya makusudi ya kumwonesha Rais wa Marekani Donald Trump uwezo wake kijeshi.

Kikosi hicho chenye askari waliofunzwa barabara kilipita mitaani jijini hapa Jumamosi wakiimba nyimbo za kizalendo huku wakiwa wamekumbatia bunduki zao zenye uwezo pia wa kurusha mabomu. 

Askari hao wanaosemekana kuwa na vifaa bora vya kivita ndani ya Jeshi la Watu wa Korea, walivalia pia miwani ya kuonea usiku iliyofungwa kwenye kofia zao za chuma huku bunduki zao zikining’inia vifuani.

“Mara tu Kamanda Mkuu Kim Jong Un atakapotoa amri, watasonga mbele kwa lengo la ‘kuuchoma mkuki moyo wa adui kwa kasi ya radi juu ya Mlima Paektu (kilele kirefu kuliko vyote nchini)’,” mtangazaji wa televisheni ya Taifa alisikika akitangaza.

Kujitokeza kwa kikosi hicho kwenye sherehe za Siku ya Jua mwishoni mwa wiki, kulikuja huku kukiwa na msuguano na Marekani na Rais Trump ambaye amekataa kukanusha mpango wake wa kuishambulia Korea Kaskazini kabla Rais Kim  hajabonyeza kiwambo cha kufyatulia makombora ya nyukilia.

Vikosi maalumu nchini viko tayari kulinda nchi hii dhidi ya majeshi ya Marekani, ambayo yanafanya mazoezi ya kumng’oa madarakani Kim mara mapigano yatakapoanza, mchambuzi wa shirika la habari la Yonhap nchini anadai.

Taarifa ya makao makuu ya Jeshi la Marekani – Pentagon, iliwaelezea wanajeshi hao wa Korea Kaskazini kama miongoni mwa waliopewa mafunzo mazuri, wenye vifaa bora, wanaolishwa vizuri na wenye motisha ya hali ya juu ndani ya Jeshi la nchi hii, CNN iliripoti.  

Ilisema kikosi hicho kisiochoonekana mara kwa mara, kinachosemekana kuendesha operesheni za siri nchini, kinaonekana kuandaliwa kwa ajili ya operesheni nzitonzito na kujilinda dhidi ya mashambuilizi kutoka nje.

Taarifa hiyo inaendelea kusema, kwamba vikosi hivyo maalumu huendesha mambo yao katika vitengo maalumu, ikiwa ni pamoja na utambuzi, mashambulizi ya angani na ya majini, makomando na utaalamu mwingine wa kijeshi.

Ilibasihiri pia, kwamba Korea Kaskazini imedhamiria kuendesha mapigano ya masafa marefu, ikitumia makombora ya nyukilia yenye uwezo wa kuishambulia Marekani moja kwa moja. 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kuzoea kuonea wanyonge kimenuka sasa

    ReplyDelete
  2. Mbona wanachelewesha kuanza tatizo nn tuone nani mkali

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kaka huko sio Somalia.kunatisha

      Delete

Top Post Ad