MREMA: JPM Niruhusu Kutoa Wafungwa Wafichue Wauaji..!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MWENYEKITI wa Bodi ya Parole, Agustino Mrema, amemwomba Rais John Magufuli amruhusu kutoa wafungwa wenye sifa ya kupata msamaha kutoka bodi hiyo ili wamsadie kufichua majambazi wanaopora na kuua Polisi.

Pia alisema ana imani majambazi wengi wanaoendesha matukio ya uhalifu wametokea magerezani au watakuwa na uhusiano na wafungwa.

Mrema alitoa ombi hilo baada ya kumalizika kwa msiba wa ndugu yake kijijini kwake Kiraracha Marangu mkoani Kilimanjaro.

Alisema kuwa ipo kampeni mbaya ya kumchafua Rais Magufuli katika utawala wake unaofanywa na wahalifu.

"Kwa uzoefu nilionao kuna kampeni chafu ya kumchafua Rais Magufuli ili nchi isitawalike kwamba hata majambazi wanaweza kuua askari hivyo kuna kila haja ya kuwashirikisha wafungwa katika tukio hili ili watisaidie kufichua,"alisema.

Aliongeza kuwa watu wabaya wasioridhika na uongozi wa Rais Magufuli wanafanya kila mbinu kwa ajili ya kumchafua ikiwemo kufadhili vikundi vya uhalifu vinavyohatarisha amani ya nchi.

Mrema alisema ili kukomesha matukio hayo ni vema Rais akaruhusu bodi yake iwakamate na kuwapunguza wafungwa magerezani hasa wale wenye makosa ya kushindwa kulipa faini ili waweze kufichua wanaohusika na uhalifu huo.

Pia alimtaka Rais kuthibiti watu wanaoleta chokochoko za maneno dhidi yake wachukuliwe hatua kwani wameonesha dhahiri hawapendeziwi na utawala wake kwani ndiyo pia wamekuwa wakifadhili matukio hayo.

Mrema alimpongeza Rais Magufuli kwa kumchagua kuwa mwenyekiti wa bodi hiyo kwani amejipanga kumsaidia kwa nguvu zote bila kujali maslahi binafsi na hadi sasa amekuwa hazifanya kazi hizo bila malipo yoyote na hana mpango wa kumdai isipokuwa atakapoona umuhimu wa kumlipa upo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad