Sumaye Azidi Kumchimba Rais Magufuli na Serikali Yake..Amefunguka Haya Mengine Kuhusu Ubora wa Mkapa na Magufuli..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


ALIYEKUWA Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, amesema kushuka kwa kiwango cha biashara nchini kunatokana na usimamizi mbovu wa sera za uchumi.

Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam hivi karibuni ambapo alisea usimamizi mbovu ni pamoja na mfumo mbovu wa ukusanyaji mapato, ambao unawafanya wahusika kuona wanatozwa kodi kubwa kuliko wanayoweza kulipa.

“Hivi karibuni tumeshuhudia kampuni nyingi zikifungwa na nyingine kupunguza wafanyakazi kutokana na kudorora kwa biashara tofauti na miaka iliyopita hali inayosababisha ugumu wa maisha na malalamiko,” alisema.

Alitaja masuala mengine yanayotishia biashara kuwa ni pamoja na vitisho mbalimbali kutoka vyombo vya dola na ukiukwaji wa mikataba.

“Kwa kiasi kikubwa kampuni zinaweza kupunguza wafanyakazi kutokana na uchumi mbovu au usimamizi mbovu wa sera za uchumi,” alisema Sumaye.

Alisema kwa kiasi kikubwa kampuni za biashara au biashara yoyote lengo lake kuu ni kutengeneza faida ambayo itatokana na biashara inayofanyika.

Aliongeza kuwa kama kiwango cha biashara kitapungua, mfanyabiashara   atapunguza gharama za biashara ambayo ni pamoja na watumishi au kufunga kabisa biashara hiyo, ili isizidi kumletea hasara.

Alipoulizwa ni nini yalikuwa makosa wakati wa uongozi wa Rais Benjemin Mkapa alisema kuwa Serikali zote huendeshwa na binadamu na siyo malaika.

“Hivyo lazima kuna mambo mema na makosa ambayo kila serikali hufanya. Muhimu ni kuwa yasiwe makosa ya makusudi bali ya utendaji ambayo yanarekebika. Wako wanaosema uuzaji wa mashirika ya umma ulikuwa makosa,”alisema na kuongeza.

“Mimi nasema siyo makosa kwani ilikuwa sera ya chama tawala ambayo Serikali na Bunge viliipitisha. Hata hivyo tukumbuke mengi ya mashirika hayo yalikuwa yamefilisika hata kulipa mishahara ya watumishi ilikuwa hailipwi kwa muda mrefu.”
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad