Mbunge Anna Tibaijuka Adai Jimboni Kwake Hakuna Shida ya Mafuta ya Taa...Tatizo Lao ni Magari Kuharibika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mbunge wa Muleba Kusini, Prof. Anna Tibaujuka amefunguka na kusema kuwa watu wa jimbo lake la Muleba hawana matatizo ya mafuta ya taa bali matatizo makubwa walionayo wao ni magari yao kuharibika kutokana na mafuta aina ya diesel kuchakachuliwa.


Tibaijuka alisema hayo bungeni baada ya kupewa taarifa na Mbunge wa Mbozi (CHADEMA), Pascal Haonga ambaye alikuwa anamwambia Tibaijuka kuwa hata wananchi wake Muleba hawataweza kununua mafuta ya taa kutokana na bei hiyo mpya kwamba itakuwa kubwa sana na kumtaka kurekebisha kauli yake, jambo ambalo Tibaijuka alilikataa na kusema jimboni kwake yeye anapigania magari ya watu yasiharibike.


"Taarifa nimeikataa kwa sababu kule kwangu sisi shida yetu ni magari yasiharibike, engine zisiharibike, kwa hiyo ngoja niwaambie mimi ndiyo nawakilisha watu wangu wa Muleba, matatizo yetu ni disel hata viwanda kama Kagera Sugar karibu kisimame kwa sababu disel inakuwa imechakachuliwa, hivyo uchakachuaji ni mkubwa. Kwa hiyo mafuta ya petroleum ilivyokaa kwenye bajeti ni sawa kabisa" alisema Tibaijuka 
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad