AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mwendesha Mashitaka wa TAKUKURU, Leonard Swai ameomba Mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa kutokana na upelelezi kutokamilika ambapo Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi July 31, 2017.
Rais wa TFF Jamal Malinzi, Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa Shirikisho hilo, Nsiande Mwanga walifikishwa Mahakamani leo wakikabiliwa na mashitaka 28, ikiwemo ya utakatishaji fedha Dola za Marekani, 375,418.
Aidha, Jamal Malinzi na wenzake, wamepata Mawakili wapya watatu kwa ajili ya kuwawakilisha katika kesi hiyo ambao walitambulishwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.
Mawakili hao ni Richard Rweyongeza, Nehemia Nkoko na Abraham Senguji ambao wanakuja siku chache baada ya aliyekuwa Wakili Jerome Msemwa kujitoa kwenye kesi hiyo kwa alichodai kutopata maelekezo yoyote kutoka kwa wateja wake.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK