Alikiba Atangaza Ujio Wake Mpya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Alikiba Atangaza  Ujio Wake  Mpya
Hit maker huyo wa ‘Aje’ amekuwa na utaratibu wa kutoa ngoma chache kwa mwaka hali ambayo inawafanya mashabiki wake kuwa na shauku kubwa ya kusikia kazi zake mpya.

Wiki hii muimbaji huyo ameanza kuibua matumani mpya kwa mashabiki wake baada ya kuanza kutoa dondoo kuhusu ujio wake mpya ambapo alipost picha katika mtandao wake wa Instagram na kuandika wananiita ‘Kipusa’.


Katika picha nyingine muimbaji huyo amepost picha na kuandika “they call me a heartbreaker?#kingkiba” kauli ambayo imewafanya mashabiki wengi wa muimbaji huyo kuwa na shauku kubwa na kazi mpya ya muimbaji huyo baada ya Diamond anayedaiwa kuwa mpinzani wake kuachia nyimbo nyingi mfululizo.

Mpaka sasa Diamond tayari ameachia wimbo, Eneka, I Miss You, Fire akiwa akiwa amemshirikisha Tiwa Savage pamoja na Marry You aliyomshirikisha muimbaji wa R&B kutoka Marekani, Ne-Yo.

Mpaka sasa Alikiba bado hajaweka wazi ni lini ataachia kazi yake hiyo mpya inayosubiriwa kwa hamu.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad