Makao Makuu ya Jengo la Yanga Kupigwa Mnada na Mahakama

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Makao Makuu ya Jengo la Yanga Kupigwa Mnada na Mahakama
Mahakama imetoa amri ya Jengo la Klabu ya Yanga lililopo mitaa ya Jangwani kunadiwa.
Hii inatokana na deni la kodi ya Majengo la Sh milioni 360 ambazo klabu hiyo inadaiwa na Serikali.

Siku ya mnada imepangwa kuwa Agosti 19 yaani keshokutwa kuanzia saa 4 asubuhi na Msolopa Investment ndiyo itakayohusika na mnada huo.
Hali hiyo inaonekana kuwashitua mashabiki wengi wa Yanga.
Mtandao huu ulifanya juhudi za kumtafuta msemaji wa Yanga Dismas Ten, simu yake iliita bila kupokelewa ndipo alipotafutwa msaidizi wake, Godlisten Anderson Chicharito na kusema yeye hafahamu chochote na atafutwe katibu wa klabu hiyo, Charles Mkwasa ndio mwenye majibu ya madai hayo.

Hata hivyo, baadaye Kampuni ya Msolopa kupitia kwa mkurugenzi wake, Ibrahim Msolopa, ilitangaza kuahirisha kwa mnada huo kutokana na makosa yaliyofanyika kabla ya kutoka kwa tangazo hilo kwani walipanga mnada huo ufanyike leo na sio Jumamosi kama ambavyo tangazo linavyosomeka magazetini.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad