AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Okwi ambaye kwa sasa yupo kwao Uganda akiwa na timu ya taifa, The Cranes, aliifungia mabao manne Simba kwenye ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa kwanza wa ligi uliopigwa Uwanja wa Uhuru, Dar.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Okwi ambaye ameyaelekeza mabao hayo kwa mkewe, amesema kuwa ataendelea kutupia mabao kadiri atakavyoweza ili kukifanya kikosi hicho kutimiza malengo yake waliyojiwekea kwa msimu huu ya kuhakikisha wanachukua vikombe watakavyoshiriki.
“Nashukuru nimeanza vizuri ndani ya kikosi changu kwa kufunga mabao haya manne, lakini kwangu mimi bado nina jukumu zito la kuhakikisha nafunga kila niwezavyo ili kuisaidia timu kufanya vizuri.
“Yaani hapa ni mwanzo tu, mashabiki wasubiri kuona nikitupia mabao mengi zaidi na zaidi kwenye kila mchezo ambao nitashuka dimbani, nafanya hivyo ili kuleta furaha kwa mashabiki wetu kwa kuwapa makombe,” alisema Okwi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK