Afisa Wa Serikali Ajinyonga Hadi Kufa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Afisa Wa Serikali Ajinyonga Hadi Kufa
Afisa mmoja wa serikali katika jimbo la Nandi nchini Kenya, Kevin Kamboi amejinyonga hadi kufa kwa kile kilichoelezwa kuhusishwa na tuhuma za uhujumu uchumi na rushwa nchini humo.

Kamboi ambaye alikuwa anafanya kazi katika Idara ya Afya kama Afisa Ugavi, aliacha ujumbe akieleza kuwa amepata msongo wa mawazo baada ya kutolewa amri na Gavana wa jimbo hilo, kuchunguzwa iwapo amehusika na vitendo vya uhujumu uchumi, huku akiwataja maafisa wenzake ndiyo waliostahili kubeba msalaba huo.
Kamanda wa Polisi wa jimbo la Nandi nchini Kenya, Peter Wambani amesema marehemu alimuomba mke wake akamuandalie kikombe cha chai huku akiendelea kutazama mpira sebuleni, lakini aliporudi hakumkuta mumewe na baada ya kumtafuta alikuta mwili wake ukining'inia kwenye mti karibu na banda la ng'ombe.
Tukio hilo limetokea huku baadhi ya maafisa wengine wa idara hiyo wamesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi, kutokana na kupotea kwa fedha za serikali.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad