Tukio la Kushambuliwa Tundu Lissu Bado Lamnyima Usingizi Wema Akesha Akilia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Tukio la Kushambuliwa Tundu Lissu Bado Lamnyima Usingizi Wema Akesha Akilia
TUKIO la kushambuliwa kwa kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida-Mashariki, Tundu Lissu ambaye ni wakili na Mwanashieria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), limewaliza wengi akiwemo staa wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu ambaye anadaiwa kukesha akilia hivyo kuibua sintofahamu kwa watu waliomzunguka.
Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa Wema ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, taarifa hizo zilimchangaya hasa ukizingatia kuwa Lissu ni ndugu yake na pia ni wakili wake katika kesi inayomkabili ya matumizi ya madawa ya kulevya.
“Taarifa za Lissu kupigwa risasi zilimchanganya sana Wema. Tangu apate taarifa hizo amekuwa akilia sana hadi kila mtu akaogopa. Tulihisi anaweza akapoteza fahamu au akapata ugonjwa hivyo tulitaka kumpeleka hospitalini, akapumzishwe,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kiliendelea kuweka wazi kwamba, baada ya Wema kuangua kilio usiku kucha na mchana kutwa, mwishoni mwa wiki iliyopita alibadilisha staili ambapo alikuwa halii, badala yake aliamua kujifungia ndani akimuombea kiongozi huyo.
“Huwezi kuamini, sasa Wema amekuwa ni mtu wa kusali tu akimuomba Mungu ampe Lissu ahueni na hali yake ilirudi kama zamani,” kilisema chanzo.
Katika kutafuta ukweli wa ishu hiyo, Ijumaa Wikienda lilimsaka Wema ili kuthibisha madai hayo ambapo alisema kuwa, hakuna kitu kilichomuuma kama hicho na bado kitaendelea kumuumiza hadi aone hali ya Lissu inatengemaa na kurudi kwenye majukumu yake ikiwemo kumtetea kwenye kesi yake.
“Naendelea kuumia hadi nitakapomuona Lissu akiwa katika hali nzuri kama mwanzoni,” alisema Wema.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad