AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Anasema kuwa washirika wa makamu wa rais Emmerson Mnangangwa wanatishia maisha ya wale ambao hawamuungi mkono kumrithi rais Robert Mugabe mwenye umri wa miaka 93.
Bi Mugabe yeye binafsi na bwana Mnangagwa wako kifua mbele na uadui wao umekigawanya chama tawala cha Zanu PF .
Mgogoro huo unajiri baada ya bwana Mgangagwa kudai kwamba aliwekewa sumu katika chakula chake mwezi Agosti.
Wafuasi wake wamesema kuwa wapinzani wake ndani ya Zanu PF ndio wa kulaumiwa, ijapokuwa bwana Mnangagwa amejitenga na madai kama hayo.
Alikiambia chombo cha habari cha taifa hilo anasalia kuwa mtiifu kwa rais Mugabe.
Bi Grace Mugabe aliyekasirika alimshutumu bwana Mnangagwa katika hafla moja mjini harare .
''Tunatishiwa usiku na mchana kwamba iwapo mtu fulani hatokuwa rais , tutauawa'', alisema.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK