Ester Bulaya Afunguka Kilichojiri Akiwa Mahabusu Mpaka Kupoza Fhamu na Kulazwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ester Bulaya Afunguka Kilichojiri Akiwa Mahabusu Mpaka Kupoza Fhamu na Kulazwa
Mbunge wa Bunda mjini kupitia CHADEMA, Ester Amos Bulaya, kwa mara ya kwanza ameelezea kile kilichojiri akiwa mahabusu mpaka kupelekea kupoteza fahamu na kulazwa.

Akizungumza na mwandishi wa habari wa East Africa Television, Ester Bulaya amesema sababu ya kukamatwa kwake ilikuwa kwa kosa la kwenda kutoa misaada kwenye shule iliyopo kwenye jimbo la mbunge mwenzake wa CHADEMA John Heche.

Ester Bulaya ameendelea kusimulia kwamba baada ya kumkamata akawaambia kwamba ana tatizo la pumu, hivyo wasimuweke kwenye mazingira ambayo yanaweza yakamletea matatizo kiafya, lakini wakamuingiza mahabusu bila kujali afya yake, na baada ya muda hali ikaanza kubadilika, na ndipo mahabusu wenzake aliokuwa nao ndani wakaanza kupiga kelele wakiwa ndani ili polisi waje wasaidie.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Midomo mirefuuuuuuuu, afya mgogoro mfyuuuuuuuu

    ReplyDelete

Top Post Ad