Mpinzani Mkuu wa Uganda Kizza Besigye Akamatwa na Polisi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mpinzani Mkuu wa Uganda Kizza Besigye Akamatwa na Polisi
Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa.

Wengine waliokamatwa pamoja na Dk Besigye, ni mgombea urais wa FDC Patrick Amuriat na katibu wa uhamasishaji Ingrid Turinawe. Wote walikamatwa jana jioni walipokuwa katika kijiji cha Burambira, tarafa ya Bubaare, Rubanda walipokuwa njiani wakielekea wilaya ya Kabale wakitokea Rukungiri.

Kamanda wa polisi wa mkoa Denis Namuwoza amesema Besigye anasakwa Rukungiri ambako inadaiwa alitenda makossa kadhaa ya uhalifu Jumatano. “Anatafutwa Rukungiri kwa kutishia kumuua ofisa wa polisi na kuandaa mkutano haramu,” amesema Namuwoza.

Ameongeza kwamba Besigye aliamuru watu kuwarushia mawe maofisa wa polisi ambao walikwenda kutawanya wafuasi wa FDC waliokusanyika kumsikiliza Amuriat aliyekuwemo wilayani kuomba kura.

Walipoondoka kuelekea Kabale saa 11:00 jioni walikutana na kizuizi cha polisi barabarani katika eneo la Burambira, kilomita nne kutoka mjini Kabale. Amuriat aliposhuka kwenye gari ili kuzungumza na polisi alikamatwa na kuingizwa kwenye gari la polisi. Kadhalika polisi walizingira gari walilokuwa wakisafiria Besigye na Turinawe.

Wanasiasa hao bado walikuwa wanashikiliwa na polisi hadi saa 1:00 usiku wakati habari hii inaandikwa.

“Bado tunamshawishi ashuke kwenye gari ili tumpeleke Rukungiri,” amesema Namuwoza
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad