Nyumba za Wabunge wa Upinzani Zashambuliwa Uganda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nyumba za wabunge wa upinzani zashambuliwa Uganda
Vitu vinavyokisiwa kuwa guruneti vimetumiwa kushambulia nyumba za wabunge wawili wa upinzani nchini Uganda, mmoja wao akiwa ni mwanamuziki ambaye sasa ni mbunge Bobi Wine, kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la nchini humo.

Polisi sasa wanachunuza mashambulizi kwenye nyumba za Bobi Wine ambaye jina lake kamili ni Robert Kyagulanyi, anayewakilisha eneo la Kyaddondo West na Allan Ssewanya ambaye ni mbunge wa Makindye West.

Mashambulizi hayo yalifanyika mapema Jumanne.
Wiki iliyopita shambulizi liliripotiwa kwenye nyumba na mbunge mwingine Moses Kasibante ambaye ni mbunge wa Rubaga North.

Wabunge watwangana makonde Uganda
Mwanamuziki Bobi Wine akamatwa Uganda
Kwenye ujumbe kupitia mtandao wa Facebook, Bobi Wine alisema kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa nyumbani kwake

Amesema amekuwa akipokea vitisho vya kuuliwa karibu kila siku.
Gazeti la New Vision lilisema kuwa wabunge ambao nyumba zao zilishambuliwa ni badhi ya wale waliotimuliwa bungeni kufuatia ghasia wakati wa mijadala kuhusu kuondolewa kwa umri wa kuwania urais.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad