Siamini Kwenye Kujichubua – Vanessa Mdee

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii wa Bongo Flava, Vanessa Mdee amedai kuwa haamini katika kujichubua ili kubadili rangi ya ngozi yake.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Kisela’ ameiambia Dj Show ya Radio One wengi wanaofanya hivyo ni wale waliokosa kujiamini.

“Mimi kama Vanessa siamini kwenye kujikoboa, kujichubua au kujibadilisha kwenye rangi yako ya kawaida au mwili wako wa kawida am belief in temporary, so ukaweka make-up au nywele kuongeza hiyo ni kitu temporary ambayo ukiamua usiku unatoa lakini vile vitu vya kufanya moja kwa moja siviamini,” amesema Vanessa.

“Na pia ile ishu ya confidence, mtu ukiwa in secured inaweza ukafanya hivyo vitu ukiwa unataka kujiboresha au kujiridhisha mwenyewe ukidhania ukijibadilisha utakuwa bora zaidi but I don’t think I need to do that,” ameongeza.

Vanessa ameendelea kwa kusema kuwa kufanya hivyo ni kinyume na imani yake na dini imekataza na anachofanya yeye ni kumshukuru kwa hatua aliyofikia sasa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad