Jeshi la Zima Moto Lafanikiwa Kuokoa Kituo cha Habari cha Clouds

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jeshi la Zima Moto Lafanikiwa Kuokoa Kituo cha Habari cha Clouds
Jeshi la zima moto limefika katika jengo la kituo cha habari cha Clouds Media Group jijini Dar es salaam, kudhibiti moto uliozuka katika mojawapo ya vyumba vya kurushia matangazo ya televisheni.
Tayari moto umeshadhibitiwa.
Sebastian Maganga, mkuu wa maaudhui na uzalishaji wa Cloud Media Group, ameiambia BBC kwamba, "moto umetokea kati ya saa tatu asubuhi hadi saa nne , athari saizi ni vigumu kuzijua. Eneo ambalo limeungua ni chumba cha kurushia matangazo ya televesheni."
Mojowapo ya vipindi vilikuwa vikuruka hewani hapo ambapo moto ulipozuka.
Pia Ambwene Mwakibete, Kaimu Kamanda wa jeshi la zima moto na uokoaji, mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, amesema kwamba
"Tumeidhibiti moto ili usimbae kwenye vyumba vingine. Tumeona ni mfumo wa kiyoyozi ambao ni umeme ndio tumeona umeathirika kwa sehemu kubwa."
Hamna majeruhi wala vifo, na thamani ya uharibifu haijafahamika bado. Chanzo cha moto hadi sasa bado hakijafahamika.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad