Serikali Kuwatetea Wapangaji wa Nyumba Kuja na Mpango wa Kulipa Kodi kwa Mwezi Mmoja Mmoja

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Kuwatetea Wapangaji wa Nyumba Kuja na Mpango wa Kulipa Kodi kwa Mwezi Mmoja Mmoja
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema kuwa iko kwenye mchakato wa kuanzisha mamlaka itakayo simamia masuala ya kodi ya nyumba itakayo fanya ukomo wa kodi kulipwa kwa mwezi mmoja na si miezi sita wala kumi na mbili.

Hayo yamezungumzwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Angelina Mabula wakati akijibu swali la Mbunge Halima Bulembo aliyehoji

Je, ni lini sasa serikali itafuta utaratibu wakulipa kodi kwa miezi 6 au mwaka na sisi kama bunge tutunge sheria itakayo walazimisha wamiliki wote kupokea kodi ya kila mwezi badala ya mwaka au miezi sita kama ilivyo sasa?

“Naomba nimtaarifu Mhe. Mbunge pamoja na wabunge wizara tayari imekwisha liona hilo, na tayari tuko kwenye mchakato wa kuanzisha mamlaka itakayo simamia masuala yote ya nyumba na katika sheria, na hiyo sheria italetwa hapa bungeni. Tumeangalia suala la ukomo wa kutoa kodi za nyumba hiyo ya miezi sita na mwaka mmoja haita kuwepo,amesema Mabula.

“Tumeona inaumiza watu wengi kwahiyo kodi itakuwa inalipwa kwa mwezi mmoja mmoja na wakati huo huo utatakiwa kuweka kama amana ya miezi mitatu kwaajili ya shughuli zingine ambazo zinaweza kuwa, kwahiyo suala hilo limelisikia na tunalifanyia kazi ,” amesema Mabula.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad