AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Tukio hilo la aina yake lilijiri wikiendi iliyopita kwenye Ukumbi wa Buckets uliopo Masaki jijini Dar ambapo katika sherehe hiyo mbali na pati hiyo pia alizindua ‘App’ yake ambayo atakuwa akiweka kazi zake zote za sanaa pamoja na biashara zake huku akipewa sapoti na mastaa wengi wakiwemo Steve Nyerere, Gigy Money, Amber Lulu, Barnaba, Aunt Ezekiel na wengine kibao.
Akizungumzia shughuli yake hiyo, Wolper aliwashukuru mashabiki wake waliohudhuria akisema: “Asanteni kwa wote mliokuja kunipa sapoti kwenye siku yangu hii.
“Nilizaliwa Desemba 6, nilisherehekea na watoto yatima.
“Lakini leo (usiku wa kuamkia Ijumaa iliyopita), nimeamua kusherehekea pamoja nanyi mashabiki wangu. “Naombeni muendelee kuniunga mkono pia kwenye App yangu ambayo nimeizindua leo.”
Hata hivyo, mbali na shamrashamra hizo, jambo lililogeuka gumzo kubwa ni gauni alilovaa mwanadada huyo.
Gauni hilo lilikuwa jeusi ambalo liliacha sehemu kubwa ya mwili wake wazi hasa katika maungo yake ya mbele kiasi kwamba alionekana kwamba kwa ndani alikuwa ametinga ‘kufuli’ pekee.
Kufuatia hali hiyo, muda mwingi Wolper alionekana akijitahidi kujiziba eneo la mbele kwa viganja vya mikono, jambo lililowafanya baadhi ya watu kuhoji kwamba kama alikuwa akiona aibu alivyovaa nusu utupu basi asingevaa hivyo!
“Sasa anafichaficha nini? Si amevaa mwenyewe? Kwa nini asiachie tu watu tuone vitu….” Alisikika jamaa mmoja aliyeonekana kudata baada ya kujionea ‘vitu’ vya ndani ya Wolper.
Hata hivyo, mbali na wengi kuonekana kuliponda gauni hilo matata, wapo waliolisifia kwamba ni mkali wa mitindo.
Chanzo: Global Publishers
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Huyu anajiuza sema nyie hamjui
ReplyDelete