Tazama Ndugu wa Babu Seya Walivyofurika Gerezani Baada ya Kusikia Wamepewa Msamaha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

BAADA ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutoa msamaha kwa familia ya Nguza Viking aliyekuwa amehukumiwa na mwanaye Papii Kocha kifungo cha maisha, ndugu wa familia hiyo na marafiki wamefurika nje ya Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam na kumshukuru Rais.

Baadhi ya marafiki wa familia ya Babu Seya wakimpongeza Mbangu.
 Mtandao huu umenasa baadhi ya picha zinazoonesha tukio zima eneo hilo hadi kuachiwa wanamuziki hao maarufu ambao tayari wameingia uraiani.

Mtoto wa Babu Seya, Mbangu Nguza (katikati) naye akiwa nje ya gereza hilo.
 “Tunamshukuru Mungu, tunamshukuru sana Rais Magufuli kwa kuwasamehe ndugu zetu. Mungu ambariki,” alisema Mbangu, mtoto wa Babu Seya.

 Babu Seya na  Papii wameachiwa leo baada ya kutumikia kifungo hicho kwa takriban miaka 13 katika Sherehe za Miaka 56 ya Uhuru zilizofanyika mkoani Dodoma hii leo.

NA DENIS MTIMA/GPL
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Furaha hii zitto zubeli kabwe WA kigoma hakupendezewa nayo na roho yake ya kolosho.

    ReplyDelete

Top Post Ad