AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akiongea na Bongo5, Baba mzazi wa Akwilina, ameishukuru Serikali pamoja na Watanzania waliojitokeza katika kuuaga mwili huo pamoja na ushirikiano huku akiwaomba Watanzania kwa ujumla kuzidi kumkumbuka.
Hata hivyo Mama Mzanzi wa marehemu alipohojiwa na Bongo5 ameshindwa kuongea lolote huku machozi yakizidi kumtoka kwa uchungu akisema hana neno lolote la kusema.
Hali ya usalama nyumbani kwa kina Akwilina kuliimarishwa na ulinzi wa kutosha kwasababu ya wingi wa watu waliojitokeza kumuaga binti huyo wakati vilio na simanzi vikitawala katika kijiji cha Marangu.
Kwa upande wa Serikali msafara wake uliondoka nyumbani kwa wazazi wa marehemu baada ya mazishi hayo yaliyofanyika majira ya Alasiri na kuwaacha baadhi ya wafiwa nyumbani kwao.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK