Kilichosababisha Moto Kuzuka Katika Mahakama ya Kisutu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kilichosababisha Moto Kuzuka Katika Mahakama ya Kisutu
Leo March 1, 2018 Kumetokea hali ya taharuki katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar Es Salaam baada ya kutokea kwa mlipuko wa moto uliosababishwa na Transfomer.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mtendaji wa Mahakama hiyo, Gasto Kanyairita amesema kuwa moto huo umetokea majira ya saa 4 asubuhi.

Amesema kuwa wakati mlipuko huo unatokea kulikuwa na kesi nyingi zikiendelea mahakamani.

“Baada ya kufatilia tulibaini kuwa ni transformer ambapo ilisababisha kuungua kwa waya wa TTCL, simu na Internet ambapo shughuli za mahakama zilisitishwa kwa muda,” -Gasto Kanyairita

Pia amesema shughuli za mahakama zinaendelea ambapo Data za kesi zipo salama.

“Niwatoe hofu Watanzania mlipuko uliotokea ni wa shoti ya umeme na ni kawaida kutokea, hivyo waepukane na taarifa za uongo,”-Gasto Kanyairita
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad