Lowasa Atinga Mahakamani Kufuata Dhamana ya Mbowe na Viongozi Wengine wa Chadema

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Lowasa Atinga Mahakamani Kufuata Dhamana ya Mbowe na Viongozi Wengine wa Chadema
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na viongozi wenzake watano wa chama hicho wamerejeshwa tena katika Mahakama ya Kisutu, Dar leo Machi 29, 2018 asubuhi ili kuendelea na kesi inayowakabili.

Mbowe na wenzake wamefikishwa mahakamani hapo wakitokea mahabusu ya Segerea ambapo wanakabiliwa na mashtaka manane yakiwemo kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha NIT, Akwilina Akwiline, Feb 16 mwaka huu, uasi na kuhamasisha chuki.

Baada ya viongozi hao kufikishwa mahakamani hapo, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa na viongozi wengine wa chama hicho walifika mahakamni hapo ili kusikiliza kesi hiyo na kufanya jitihada za kuomba dhamana kwa watuhumiwa hao leo.

Viongozi wengine waandamizi wa chama hicho wanaoshtakiwa katika kesi hiyo ni: Katibu Mkuu Dkt Vincent Mashinji, John Mnyika, Salum Mwalimu, Mch. Peter Msigwa na Ester Matiko ambapo wote wamefikia kwenye chemba ya mahakama panaposikilizwa kesi hiyo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad