Harusi ya Alikiba Ukumbi/Mapambo Yagharimu sh milioni 40 za Tanzania

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwandishi wetu aliyepo Mombasa, Mohammed Ahmed anaripoti kuwa mapambo katika ukumbi uliofanyika sherehe hiyo yamegharimu Sh2 milioni za Kenya ambazo ni wastani wa Sh40 milioni za Tanzania.

Mpambaji wa ukumbi wa Diamond Jubilee unaochukua watu 1,500 katika jiji hilo ambaye mwandishi wetu alimkuta akiendelea na kazi, anasema amelipwa kiasi hicho cha fedha ambacho ni kikubwa kulingana na aina ya mapambo waliochagua maharusi.


Inaelezwa kuwa familia ya binti huyo ina uhusiano wa karibu na Gavana wa Mombasa, Hassan Joho ambaye ni rafiki wa Alikiba.

Inaaminika kuwa Joho ndio amesaidia kwa kiasi kikubwa kumuunganisha Kiba na familia ya Amina, ambapo safari zake za mara kwa mara mjini Mombasa, hazikuwa kwa shughuli za kimuziki tu bali ni kuwa karibu na mkewe huyo mtarajiwa.

Harusi hiyo imefanyika jana Mombasa ambako Joho na vigogo wengine wa Muungano wa NASA walihudhuria 

Chanzo: Mwananchi
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad