AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Simba inatarajia kukutana na Prisons leo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar katika mchezo wa Ligi Kuu Bara.
Simba ambayo inaongoza msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi 55, kama ikishinda leo itakuwa imeiacha Yanga kwa tofauti ya pointi 11 lakini Yanga ikiwa na michezo miwili mkononi.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Kichuya alisema kuwa mechi yao na Prisons ndiyo itakayoamua ubingwa wa Simba kwa kuhakikisha wanashinda mchezo huo kwa hali na mali.
“Mechi yetu na Prisons ndiyo itakayoamua ubingwa wetu msimu huu tukifanikiwa kuwaumiza wao tutakuwa tumejiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kutwaa ubingwa.
“Tukimaliza mechi hiyo tunaangalia mechi ya wale wenzetu wa upande wa pili, tunahakikisha tunawafunga ili tunyakue ubingwa rasmi,” alisema Kichuya
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK