AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
La Liga ni ligi kubwa Ulaya ambapo mastaa mbalimbali wanacheza wakiwemo Lionel Messi wa Barcelona na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya Simba, kimelipasha Championi Jumamosi kuwa, kuna timu kubwa kutoka Hispania ambayo imepanda ligi kuu inamtaka Kapombe alipokuwa akiichezea Simba mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Masry ya Misri baada ya kuvutiwa na uwezo wake.
Championi Jumamosi lilimtafuta Kapombe ili aweke wazi kuhusiana na taarifa hizo, ambapo alisema: “Nikweli kuna mawakala zaidi ya watatu wamenipigia hivi karibuni wakinitaarifu uwepo wa timu zaidi ya tatu kunihitaji.”
“Wakala wa kwanza ameniambia kuna timu ya Hispania inanitaka, lakini pia zipo zingine mbili, moja kutoka Urusi na nyingine ipo Bara la Asia ambazo zote nimeshataarifiwa kunihitaji, hivyo wakala wangu ameniomba nitume tu baadhi ya ‘clip’ (video) zangu ili aweze kukamilisha dili hilo.
“Hii ni bahati sana kwangu kuonekana kwa muda mfupi huu ambao nimecheza Simba, japo nia yangu ningependa kuendelea kuwa hapa ili nijiweke vizuri zaidi kwani nina malengo mengi sana ambayo bado sijayafikia pamoja na kwamba wao wameshaona uwezo wangu,” alisema Kapombe.
Stori: Musa Mateja, Dar es Salaam
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK