Mo Salah atacheza World Cup? Daktari wa timu atoa neno hili.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mtanange wa yule Bingwa wa Ulaya umekamilika. Real Madrid wameshinda taji lao la tatu mfululizo kwa ushindi wa mabao matatu kwa moja. Golikipa wa Liverpool Karius akisababisha uzembe ulioigharimu timu hao baada ya kurusha mpira kimakosa na ukagomga Benzema aliyegfunga bao la kwanza kabla ya Mane kusawazisha. unga magoli mawili. Bale alitokea benchi na kufunga mabao mawili.



Niliwahi kusema kinyago cha Gazzaniga (Kombe la Dunia) kiliwanyima mastaa wengi usingizi. Majeraha ilikuwa changamoto kubwa sana kwa wachezaji wa pande zote.

kilichotokea leo ni kitu ambacho wengi tulitarajia kutapoteza ladha ya mchezo huu.



Mo Salah ambaye alikuwa mchezaji tegemezi wa Liverpool hivi leo atolewa kwenye mchezo mapema kabisa baada ya kuumia bega. Ilikuwa ni kashkash kati yake yeye na Sergio Ramos. Ramos alikwenda kumkaba Salah na ilionekana wakishikana mkono. Picha na video zinaonesha kuwa alimvuta mkono na kumsababisha Salah kuondoka vibaya na kulalia bega lake.



Je wachambuzi wakubwa wanasemaje?

Rio Ferdinand
Ramos amekaba vyema. Alifanya kitu ambacho mlinzi yeyote angefanya. Sidhani kama alidhamiria.

Frank Lampard

mnapokuwa mmesogeleana sana mara nyingi ni rahisi sana kushikana mikono. ile ni bahati mbaya sana.



Rio na Lampard hawa ni waingereza na wana haki ya kutoa Maoni yao. Jana nilimsikia David Beckham aliweka pembeni sana suala la Uzalendo. Na aliweka mapenzi yake dhahiri kuwa Real inafaa iifunge Liverpool. Rio nae ni hasimu mkubwa wa Liverpool. Bila shaka ukiangalia ile video utagundua hakuna ajali. kuna tofauti kubwa ya kushikana na kumvuta mtu kwa makusudi ukidhamiria.



John Simpson anasema hivi

Nimeangalia maoni ya wachambuzi wakubwa, wanasema lile tukio ni ajali. Sawa. Lakini ukimwangalia Ramos wakati Salah anatolewa nje utagundua alidhamiria.



kuna baadhi ya video zinamuonesha Ramos akitabasamu na Mwamuzi wa pembeni.

David Maddock anasema

Inauma sana. Ramos amefanya kitendo cha kikatili haswa. Hajaharibu tu ndoto za Salah za Uefa pia huenda ameharibu ndoto wa Wamisiri wote.



Mo Salah taarifa zinasema mishipa ya bega imeachana. Na majibu kamili yatatolewa wakirudi jijini Liverpool. Hii inaleta wasiwasi mkubwa kama atahitaji kufanyiwa upasuaji. na itamlazimu kukosa michuano ya kombe la dunia.



hata hivyo taarifa za hivi punde zinasema kuwa ukurasa wa timu ya taifa ya Misri umeweka taarifa kuwa Mo Salah atacheza michuano ya kombe la dunia

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad