AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akichat Live na wananchi kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kila Jumatano kupitia ukurasa wa Facebook EATV, Musukuma amesema kwamba viongozi wengi wanaojinasibu kuwa wana elimu kubwa ukikaa nao karibu matendo yao hayafanani na viwango vya elimu wanayoisema.
Aidha Msukuma amefafanua kwamba ifike mahali watu wawe wanawajaji wenzao kwa matendo yao na siyo vyeti kwani watu kuamini kwenye vyeti ndiko kunakopelekea watu kwenda kufoji mpaka vyeti.
"Mimi nafahamu mule bungeni kati ya Wabunge 360 Wabunge 180 ni darasa la saba japokuwa hawataki kueleza ukweli. Wametegesha vyeti ili wapate uwzairi. Unamkuta mtu anavyeti ambavyo huko nyuma hakuwa navyo. ukifatilia historia kabla ya kuingia bungeni alikuwa Jobless wengine ma DJ na elimu wanazizisema sijui Cambridge hawana".
Pamoja na hayo Musukuma amesema pamoja na kuwa alisha declare yeye ni darasa la saba ipo siku ataweka wazi kiwango cha elimu yake na kwamba licha ya kuwa ana elimu hiyo yeye ni mtu ambaye anapenda kusoma na ana uelewa wa kupambanua mambo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK