“Sijaongea na familia ya Masogange” - Belle 9

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii wa muziki nchini Abelnego Damian, maarufu kama Belle 9, amesema kuwa bado hajaongea na familia ya msanii marehemu Agnes Gerard “Masogange” kuhusu kumsaidia mtoto wa marehemu kwasababu hakuwa na ukaribu na familia hiyo.


Belle 9 amesema hayo jana Mei 25, 2018 katika kipindi cha FRIDAY NIGHT LIVE kinachorushwa na EATV kila siku ya Ijumaa saa 3:00 usiku na kuongeza kuwa aliifahamu familia ya Agnes Gerard “Masogange” baada ya kutokea msiba hivyo imekuwa ngumu kwa yeye kuwasiliana nao.

“Sijapata nafasi ya kuongea chochote kwasababu hatukua karibu sana na pia hakuna mtu alitarajia, kwahiyo sijaongea chochote kuhusiana na mambo ya familia kwamba nitafanya chochote kuhusu yule mtoto” amesema Belle 9

Belle 9 ameongeza kuwa alihuzunika sana kutokana na kifo cha msanii huyo kwasababu ya ukaribu waliokuwa nao, pia “Masogange” alichangia kwa kiasi kikubwa katika mafanikio yake ya muziki baada ya  kushiriki katika video ya wimbo wake wa “Masogange”.

Marehemu Agnes Gerard alipata umaarufu baada ya kushiriki  katika video ya wimbo wa msanii Belle 9 ulioitwa “Masogange” mwaka 2009.

April 20, 2018 Agnes Gerard “Masogange” alifariki Dunia Jijini Dar es salaam baada ya kuzidiwa na homa ya tumbo na upungufu wa damu na alizikwa nyumbani kwao Utengule-Mbalizi Mkoani Mbeya April 23, 2018.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad