Vilio Simanzi Vyatanda Kuagwa Miili ya Watumishi Watatu wa TIC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Vilio Simanzi Zatanda Kuagwa Miili ya Watumishi Watatu wa TIC
Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage ameungana na mamia ya waombolezaji kuaga miili ya watumishi watatu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) katika ukumbi wa Karimjee jijini hapa.

Watumishi hao meneja wa tafiti na miradi, Martin Masalu, kaimu mkurugenzi wa tafiti, Alvin Said Amir na kaimu mkurugenzi wa uhusiano walifariki dunia Mei 21, 2018 kwa ajali wakati wakitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma.

Akizungumza leo Alhamisi Mei 24, 2018  Mwijage amesema Taifa limepoteza nguvukazi, “kubwa walilolifanya vijana hawa ni kuhakikisha Watanzania wanawekeza ili wasiwe watazamaji na kwa kweli vijana hawa wamejituma na  ni wachapakazi.”

Huku akiwaomba watumishi wa kituo hicho kuchapa kazi licha ya kuwapoteza wenzao  amesema, “msije mkasema hao wameondoka pengo lao haliwezi kuzibika, fanyeni kazi kama wao huu mzigo ni wenu sasa.”

Mwijage ametoa pole kwa wawekezaji nchini kwa kupoteza watu ambao wamawazoea.

Watu wa kada mbalimbali walishiriki kuaga miili ya watumishi hao.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad