Unaikumbuka Hii.....Barua ya Mfungwa Papii Kocha kwa Rais JK.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

BARUA YA PAPII KOCHA
KWA RAIS
JAKAYA KIKWETE... KWA
WALE
AMBAO HAMJAISOMA HÍI
HAPA.
MF/NA: 836'04
Johnson Nguza
(Papii Kocha)
Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es Salaam
Mh. Rais Jamuhuri ya
Muungano
Tanzania
YAH: MAOMBI YA
KUPEWA MSAADA
(MSAMAHA) WA
KUFUTIWA ADHABU
YA KIFUNGO NILIYOPEWA
NA
MAHAKAMA YA HAKIMU
MKAZI
KISUTU.
Husika na somo hilo hapo
juu.
Mimi ni mfungwa katika
gereza
kuu Ukonga. Kwa heshma
na
taadhima na kwa
kutambua utu
na huruma yako ya
kiMUNGU
ulionayo dhidi ya
binadamu
wenzako pamoja na
mamlaka
uliokabidhiwa na Jamuhuri
ya
Muungano wa Tanzania.
Naanguka na kushika
miguu yako
mitukufu muheshimiwa
rais.
Nakuomba msaada
(msamaha)
kwako muheshimiwa
rais, kwa
njia hii ya maandishi
kusudi
niweze kuondolewa
adhabu ya
kifungo cha maisha
gerezani,niliyohukumiwa
na
mahakama tajwa hapo
juu.
Mh.Rais mimi
nimefungwa nikiwa
bado kijana mwenye umri
mdogo,
na ukweli kutoka moyoni
sikufanya kosa hilo. Si
mimi, baba
yangu Nguza wala ndugu
yangu
yeyote aliyefanya
kitendo kile.
Lakini wenye mamlaka
wakatuona tuna hatia na
kuamua
kuteketeza kizazi chetu
gerezani.
Natamani kiama ifike ili
mwenyezi
Mungu aweke wazi
ukweli wote
uliojificha nyuma ya pazia.
Mpaka
sasa natambua wazi
hatima
pamoja na dhamana ya
maisha
yangu ipo katika mikono
yako
mitukufu Mh. Rais
Naomba huruma yako
muheshimiwa Rais
maana mimi ni
mtoto wako ninaehitaji
huruma
yako wewe mzazi. Lakini
pia sisi
ni binadamu wenye nafsi
na miili
kama wengine.
Waliotumia mamlaka yao
kutuweka gerezani nao ni
binadamu pia, wenye miili
na
nafsi. Ipo siku nafsi zetu
zitapaswa kutoa hesabu
ya
tuliyoyafanya hapa
duniani.
wakati huo miili yetu
tunayoitumia
kunyanyasa
wanyonge itakuwa
imeoza
mavumbini.
Natumaini kauli yako ya
mwisho
ndio itakayoleta pumzi ya
uhai
nafsini mwangu.
Nakutakia kazi
njema, afya njema na
maisha
marefu.
Mungu akubariki.
Wako mtiifu
Mfungwa NO:836'04
JOHNSON
NGUZA (PAPII KOCHA)
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Maskin jaman dah mpaka mwili unasisimka....wasamehewe jaman,,

    ReplyDelete
  2. hakuna cha madaraka kwa aliye juu(mola), kwani raha wanazofarijika nazo kwa kunyanyasa wengine itakuwa kilio na kusaga meno. "mungu awe nanyi papii na familia yako"

    ReplyDelete
  3. Inshaallah Mungu amtie huruma raiswa jamuhuri ya TZ.. Natoa pole na mlalamishi na Mungu akupe subra.. Utasemehewa inshallah na Mola akufungulie milango ya neema..Ameen.

    ReplyDelete
  4. Mi nadhani wangeweka wazi kwenye media nani ambaye aliwafanyia unyama wa kuwasingizia,ilikuwaje mpaka wakawa na bifu na huyo mkubwa ......kila mtu anasema lake...sasa ni wakati wa kuweka mambo hazarani ili wananchi tujue ukweli ...papii kocha funguka jamii ijue

    ReplyDelete
  5. Mungu atatoa hukuku yake Inshaalah kama kweli hamna hatia nawatakia kila la kheiri tumemiss sauti yako

    ReplyDelete
  6. kiukweli inatiauruma mh rais sikiliza vilio vya wanyonge machozi yao yatafutwa nani?

    ReplyDelete
  7. maskini inasikitisha sanaa, mungu awatie nguvu, Mheshimiwa wasikilize jamani wameteseka vya kutosha. familia nzima imepoteza matumaini, Tunakuomba baba yetu uwasidie mungu atakubariki,

    ReplyDelete
  8. yahh kweli anahitaji msamaha

    ReplyDelete
  9. Mhe. Rais Kikwete naomba usikilize kilio cha huyu kijana umsamehe si yeye tu hata hao aliowataja.

    ReplyDelete
  10. So! So! Sad,Mwenyez Mungu awape moyo wa subira asipokusamehe binadam Mwenyez Mungu anasamehe Insha'allah polen sana ukikosa fungu duniani utalipata kwa Allah.WASIJISAHAU NAO NI BINADAM Mungu atatenda haki juu yao wamezishika sheria za nchi nasi za Mbingu.Rily sad!

    ReplyDelete
  11. Asisamehewe si alitenda uchafu wake.kizazi chote kiishiee jela.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mungu akusamehe bure maana si ajabu wahusika wakuangamiza wengine ndo nyie.ila kumbuka kipimo upimiacho wengine nawe utapimiwa tu!!!!!!!!!!!!!!!!

      Delete
  12. NAJUA RAIS TULIE NAE SASA HANA HAYA YA KUTUMBUA MAJIPU. NAOMBA HILI LA HII FAMILIA YA NGUZA ASILIFUMBIE MACHO KAMA HAKI HAIJATENDEKA MUNGU YUPO ANAYEONA WANYONGE, RAIS WA AWAMU HII YA TANO NAOMBA UFANYE ZIARA YA KUSTUKIZA PIA KWENYE VYOMBO HIVI VINAVYOHUSIKA NA KESI HII YA FAMILIA HII ILI WAWEZE KUSAIDIKA

    ReplyDelete

Top Post Ad