Picha za Mama Aliyekaa Juu ya Paa kwa Siku Tano Kuzuia Nyumba Kuuzwa na Bank

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Huyu mama alikaa juu ya paa kwa siku tatu tangu jumamosi kupinga nyumba yao kuchukuliwa na bank.Anasema mumewe alimdhamini mtu alipochukua mkopo bank miaka mingi iliyopita na kushindwa kulipa mkopo huo.
   Kwa mujibu wa maelezo yake kesi yao bado ipo mahakamani kwani tayari yule mdaiwa kuna mali zake zilizotaifishwa.
Mdaiwa alikopa ml 240 wameuza nyumba zake 2 na mabasi mawili.Wenyewe wanachodai katika hilo deni imebaki tsh ngapi na wao watoe?kama nyumba iuzwe watoe deni la bank na hela inayobaki wabaki nayo wao.

Nyumba ipo mbezi Tangi bovu na inaeneo kubwa sana mama anasema hata akiuza si chini ya ml 500 iweje atolewe kwa ml 240?wakati mdaiwa nyumba zake mbili zimeshachukuliwa na mabasi mawili yale makubwa ya safari za mikoani.Hiyo ml 240 haijatimia tu?na kama bado kiasi gani kimebaki?

 Ndani ya nyumba vitu walishachukua hao watu wa auction mart  ndani kweupe.Na wakati haya yakiendelea hakukuwa na amri yoyote iliyotoka mahakamani wala hawakuwa na kibali cha mahakama.
Gea alimfata huko huko juu kumsikiliza na tumemsikia leo kwenye heka heka.Kesho pia itaendelea...

 Chumba cha habari cha clouds fm kimeenda kufatilia hapo bank ya Tanzania Investment bank(TIB)kujua kulikoni??
Maana wakati haya yakiendelea hiyo jana inasemekana hii nyumba imeshauzwa.Inauzwaje na shauri lipo mahakamani?Na jana mume wa huyu mama alikuwa mahakamani maana ilikuwa siku ya kesi kuendelea kusikilizwa.
Na mumewe alirudi na oda maalum kutoka mahakamani kuwa nyumba hiyo isiguswe na vitu vyao virudishwe.

Source:Dinamarios  Blog


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

5 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. DUH NINGEKUWA NA MKE JASIRI NAMNA HII NINGEMPA TUZO AMBAYO ASINGESAHAU MAISHANI

    ReplyDelete
  2. Huyu ndio mke!

    ReplyDelete
  3. Niwazi anamchango mkubwa km mke ktk hiyo nyumba angeikuta asingesimama kuhakikisha nyumba haiuzwi.. Dah ww nimwanamke???

    ReplyDelete
  4. Komaa!,safi sana.

    ReplyDelete

Top Post Ad