UTAJIRI WA MASANJA MKANDAMIZAJI NI HATARI TUPU...DIAMOND NA JIDE CHA MTOTO

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

UTAJIRI wa komediani maarufu nchini  Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ ni kufuru! Tena unatisha na sasa anaonekana kuwa miongoni mwa wasanii wanaomiliki fedha na mali nyingi Bongo, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.

Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ akiwa mbele ya usafiri na mjengo wake.

HABARI MEZANI

Awali, habari kuhusu utajiri wa Masanja ilitua mezani mwa gazeti hili kama kidokezo, hapo mwandishi wetu akaingia mzigoni na kuanza kuchunguza kwa kina mali anazomiliki msanii huyo na kugundua kuwa ni kati ya mastaa mabilionea Bongo.

“Masanja sio yule tena. Ana mpunga (fedha) mrefu sana. Hakuna msanii wa maigizo Bongo anayeweza kumfikia kwa sasa. Hao wengine ni mbwembwe tu, lakini pesa imelala kwa Masanja,” kilipasha chanzo chetu.

Kikaongeza: “Kwanza ana ghorofa lipo Tabata, hapo ndipo anapoishi. Pia ana magari kibao ya kifahari, mashamba ya mpunga na Kampuni ya OK Security inayolinda sehemu mbalimbali zikiwemo taasisi nyeti nchini.

Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ akiwa kwenye pozi na miongoni mwa magari yake.

“Ni msanii gani mwenye kampuni kubwa kama ya Masanja? Wengi wanaishia kudai wanatayarisha filamu ambazo hata matunda yake hayaonekani.”

Uchunguzi wetu ulibaini ukweli wa mali za msanii huyo na mambo mengine mengi yanayoingia kama vyanzo vya mapato yake.

MAGARI SITA

Ilibainika kuwa, Masanja anamiliki magari sita, yakiwemo ya kifahari. Baadhi ya magari hayo ni Toyota Land Cruiser V8, Nissan Hardboad na Toyota Verossa.



NYUMBA TATU BONGO

Pia, mkali huyo wa kuvunja mbavu, anamiliki nyumba tatu za maana jijini Dar es Salaam, moja ni ghorofa ipo Tabata, nyingine Kigamboni na nyingine haifahamiki eneo rasmi ilipo.

Hata hivyo, imebainika kuwa mbali na mijengo yake hiyo iliyopo jijini Dar, nyumbani kwao Mbarali, Mbeya ana mjengo wa maana.



MASHAMBA KIBAO

Msanii huyo hayupo nyuma kwenye kilimo, ana mashamba kadhaa Kigamboni jijini Dar es Salaam lakini linalotia fora ni lile lililopo Mbarali lenye ukubwa wa hekari 50 ambalo analima mpunga.



NI MSANII WAMAIGIZO TAJIRI ZAIDI?

Kwa utajiri huo, ipo minong’ono kuwa, nyota huyo anaweza kuwa kwenye namba za juu za wasanii wa maigizo wenye mkwanja mrefu.

Wengine wanaotajwa kwenye orodha ya waigizaji matajiri Bongo ni Husna Posh ‘Dotnata’, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ na Amri Athumani ‘Mzee Majuto’.

MATAJIRI BONGO FLEVA

Katika muziki wa Bongo Fleva, wasanii wanaoaminika wana utajiri mkubwa zaidi ni Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Joseph Haule ‘Profesa Jay’.

Wasanii hao wanamiliki mijengo ya maana, achilia mbali magari ya kifahari na miradi kadhaa.



MASWALI KUHUSU MASANJA

Utajiri wa Masanja umeonekana kuibuka ghafla huku vyanzo vyake vya kumwingizia kipato vikijulikana ni sanaa ya uigizaji, muziki na huduma ya uchungaji.

Je, kwa uigizaji tu katika Kundi la Orijino Komedi ‘OK’ ndiko alikopata mkwanja huo na kuanzisha miradi hiyo mikubwa?

Kama ndiyo, kwa nini memba wenzake ndani ya kundi hilo hawana maendeleo makubwa kama yeye?

Kazi nyingine ya Masanja ni muziki wa Injili ambapo kwa sasa albamu yake ya Hakuna Jipya iko sokoni. Je, albamu hiyo na shoo anazofanya zinaweza kuwa chanzo cha utajiri huo?

Lakini pia Masanja ni mchungaji ambaye anahudumu katika Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT) ‘Mito ya Baraka’ lilicho chini ya Askofu Bruno Mwakiborwa. Je, mshahara anaoupata kutokana na huduma hiyo unaweza kuwa chanzo cha mapato yake?

Risasi Mchanganyiko halikutaka kupasua kichwa, juzi lilimsaka Masanja kwa simu na kumhoji juu ya mali zake ambapo kwanza alithibitisha kweli anamiliki mali hizo na nyingine ambazo hakupenda kuzitaja.

“Ni kweli nina nyumba tatu hapa mjini, kampuni ya ulinzi na mashamba ya mpunga eka 50 nyumbani Mbarali, Mbeya. Kuhusu magari pia ni kweli kabisa. Mimi ni mtumishi sitakiwi kusema uongo,” alisema Masanja.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

24 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Huyo ni freemason mbona anafahamika.

    ReplyDelete
    Replies
    1. nikisema Nana J mmbeya.Haya !!!!!Bye sitaki lawama mie ndo ilivyo hivyo.

      Delete
    2. Uko serious kabisa mwanaume mzima na mboo inadinda, kuweni na wivu wa wa maendeleo acheni majungu

      Delete
  2. Masanja hatari, tuambie siri ya mafanikio.

    ReplyDelete
  3. Alafu huyu jamaa ni mchungaji gani? anayesokota nywele sipati jibu.wadau mnasemaje.

    ReplyDelete
  4. Achen upumbavu watu wanajishughulisha usiku na mchana wakifanikiwa mnasema freemason,umeambiwa anaigiza,anahubiri,ana shamba la ekari 50analima,ana kampuni ya ulinzi ,hivyo vyanzo vyote bado unasema freemason,fanyeni kazi kuliko kubanana mjini mnalia kazi hamna.

    ReplyDelete
  5. Mdau 2:05, Hapo ni wizi mtupu.

    ReplyDelete
  6. Lakin huyu br, anajituma sana

    ReplyDelete
  7. Hakuna freemason kwa masanja ,hizo ni juhudi binafsi,jitume ktk kazi utafanikiwa,undeni vikundi mkopesheke au njooni huku mgodini mfanye kazi.,mafanikio hayaji bila kujituma.

    ReplyDelete
  8. Nasikia anajiuza china

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama anajiuza china nenda kajiuze tuyaone mafanikio yako

      Delete
  9. Bidii ndo mafanikio,huwezi ukapiga hatua nje ya mipaka ya ufahamu wako,wanoamini ili uendelee mpaka uwe freemasons ni vigumu sana kufanya kazi wakapiga hatua,na watanzania tumekuwa limbukeni wa kuamini kuwa mtu hawezi kuendelea bila freemason,hata wewe ukijushughulisha ukanunua hata gari lazima waseme freemason,ingieni kwenye mtandao muulize maana ya freemasons.

    ReplyDelete
  10. diamond endelea kuuza sura tu mjini wenzio wanatengeneza hela,endelea tu kubadilisha wanawake kama chupi

    ReplyDelete
  11. Kontena hilo!

    ReplyDelete
  12. Asa hapa diamond kaingiaje we comment mada iliyopo diamond we2 muache ovyooooo mxxxxxxxxxccci

    ReplyDelete
  13. hakuna mtu anae mtegemea mungu akaaibika mtabaki kusema ni freemason kumbe mwenzenu kabarikiwa...even bible inasema hakuna mwenye haki alie chin yangu akaiabika milele...acheni kuchuma dhambi za bure jaman .....uongo ni dhambi free mason ulimwona na kama wasema hivo bac na we ni mwanachama....

    ReplyDelete
  14. Diamond acha midomo domo oooh..nnna nyumba tisa..tako wewe nyumba tisa unapanga.?endelea kugawa mkundu tu na kujisifia watu wanapiga hela kiukwelikweli.

    ReplyDelete
  15. We msenge kwel asa domo hana ela???!!hyo mmeambiwa ni kwa upande wa maigizo ila ukiwachanganya wote domo bdo yupo juu....nawapenda wote lkn shemeg domo na masanja

    ReplyDelete
  16. mchumgaj gani ana ana rasta kam dekio la gesti kuma uyoo

    ReplyDelete
  17. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  18. UTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASIRI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI ZAKE NA KIFUATA MIONGOZO YAKE...... NDAGU NI NINI?
    Ndagu ni aina ya dawa ya kufanya jambo lolote kwa kupewa mtihani au jaribio fulani haswa kutoa sadaka(wanyama, kiumbe chenye chenye roho halisi hai ( piga;0742162843 ndio utanielewa au utakuwa umenielewa) au kutimiza sharti fulani ili kupata mali. Ndagu huofautiana nikimaanisha zipo aina tofauti zilizo na masharti nafuu na zenye masharti magumu kulingana na thamani ya damu ambayo inatolewa.
    DR MDIRO ANAKULETEA AINA 6 ZA NDAGU
    1.KUTOA SWADAKA YA KIUMBE CHA MIGUU MIWILI (0742162843)
    2. MIMBA (karibu kwa maelezo zaidi usifikirie ukapotea kwa mawazo tofauti)
    3. UTASA
    4.NDUGU WATATU ( hapa utaratibu sio damu yako karibu kwa maelezo zaidi)
    5.ULEMAVU ( kwa hii ni kuwa MTU anajiswadaka mwenyewe 0742162843 kwa maelezo)
    6.WANYAMA (damu za wanyama wenye thamani kwa hili ni aina tatu "mbuzi,kondoo na Ndama")

    (KWANINI USUMBUKE)
    NAITWA DR, MDIRO
    piga;0742162843. 
    KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU ULINZI KWA MALI YAKO (HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)

    NDOA, AU KUMVUTA UMPENDAE,MIKOSI,MABALAA, 
    JINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI. NIPIGIE 0742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA KWA UMAKINI NA KUFATA MASHARTI.

    (kuhusu utajiri au pesa
    za ndagu/majini)
    KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+ na kuendelea
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri 
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote.

    ASANTE.....KARIBU.

    ReplyDelete

Top Post Ad