Video Nzima Edzen Jumanne Akeleza Jinsi Ndoa Yake na Dida Ilivyovunjika, Kumbe Big Brother Ndio Tatizo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Stori: Deogratius Mongela na Chande Abdallah

SIKU chache baada ya kuvunjika kwa ndoa ya Khadija Shaibu ‘Dida’, aliyekuwa mumewe, Mtangazaji wa TV1, Ezden Jumanne ameibuka na kutoa sababu kuu tatu za kutengena kwao, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.

Akizungumza na waandishi wetu katika nyumba aliyohamia kwa sasa, Kijitonyama, Dar, Ezden alisema mgogoro kati yake na Dida ulianza zamani ambapo Dida alikuwa na tabia ya kurudi usiku mnene, Ezden alidai kadiri siku zilivyozidi kusonga mbele, tabia hiyo ilizidi kuonekana ingawa alikuwa akimuonya mara kwa mara.

BIG BROTHER NDIYO TATIZO
Pamoja na sababu hizo, Ezden aliitaja sababu kuu iliyoanza kuzua mgogoro uliosababisha kuvunjika kwa ndoa hiyo ni Shindano la Big Brother Africa linalotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu nchini Afrika Kusini.


Alisema siku moja mtalaka wake huyo alimweleza kuwa kuna rafiki yake aliyemtaja kwa jina la Furaha amempa mchongo wa kuwa mgeni staa (celebrity guest) ndani ya Jumba la Big Brother na kumuomba ampe ridhaa ya kwenda huko.

Akizidi kumwaga data mbele ya kinasa sauti cha Risasi Mchanganyiko, Ezden alisema:
“Nilimruhusu kwa moyo mmoja ambapo pia aliniomba nimsaidie kumpa uzoefu juu ya lugha ya Kiingereza ili akaendane na kanuni za Big Brother.

“Kama mume nilimsapoti kwa nguvu zote, siku nyingine kama nikiwa nimerudi nyumbani mapema mimi mwenyewe nilikuwa nikimfundisha ‘tense’ mbalimbali.”
Katika aya nyingine, Ezden alisema kuna siku Dida alimfungukia kuwa hatakwenda Big Brother kama mgeni staa kwani anatakiwa kuingia kama mshiriki na kumwambia kuwa alikuwa akiogopa kumwambia ukweli mapema.

“Nilimkatalia ndipo alipocharuka, huwezi amini alifikia hatua  ya kusema nambania zali lake. Niliumia sana siku ile ikabidi nimuulize kama anaithamini Big Brother kuliko ndoa yake, hakunijibu.
“Kama mume ilibidi niwaulize wazazi na mashemeji zangu kama wamemruhusu Dida kushiriki shindano hilo kama alivyoniambia, walidai aliwaambia kuwa mimi ndiye niliyemruhusu ndiyo maana nao hawakuwa na pingamizi.

“Baada ya kuwaelewesha waliniambia hawakupenda mambo hayo ya Big Brother kwa kuwa yana udhalilishaji ndani yake,” alisema Ezden.
Siku ya tukio, Ezden alisema alikuwa akioga bafuni na simu yake ilikuwa kitandani, ghafla Dida alimfuata na kumuuliza kwa nini aliweka password!

“Alipiga kelele mpaka majirani wakaanza kujaa nyumbani kisa ‘password’ niliyoiweka kwenye simu yangu. Nikamuuliza yeye si ndiye aliyesema kuwa kila mtu awe na simu yake! Akaanza kunipa maneno ya kejeli.
“Hapo nikaona heshima yangu inashuka. Kiukweli nilimpiga mpaka nikamuumiza. Baadaye akaondoka kwa hasira kumbe alikwenda kuwachukua ndugu zake.

“Walipokuja tukajitahidi kusuluhisha lakini kila nilipopewa nafasi ya kuzungumza, Dida aliniingilia. Kwa kuwa tulishawahi kukaa vikao vingi sana kabla lakini hakuna tulichoweza kusuluhisha, niliona hakuna  haja ya kuendelea naye,” alisema Ezden na kuongeza kuwa kikao hicho kiliisha kwa ahadi kwamba angetoa talaka kwa Dida ambaye naye alionekana kuikubali.

Ezden alisema, Juni 28, mwaka huu  alimpa Dida talaka tatu na kuongeza kuwa hategemei kurudiana naye wala kuoa hivi karibuni.Kwa upande wake, Dida alipopewa nafasi ya kuzungumza alisema: “Mimi sina la kusema na wala sitaki kulumbana na mtu.
GPL
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

29 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Dida aibu!!! Umri hio bigbrather?? Ukakae uchi huko mtoto wa kiislam? Lol,au unajionatoto kwakua uliolewa na mtoto?! Yani AIBU! Kweli ww kurumbembe umembaka mtoto wa watu stil unataka aishi km bushoke? Ila dis time umewezwa msomi huyo na anajielewa kakutwisha talaka tatu hataki shobo! Malaya usokua na huruma na watoto wa wanawake wenzio!? Lol eti bigbro uzee hio dida ww c 35 yrs old mamaaa unataka ukamuaibishe mumeo!? Dah so sad...

    ReplyDelete
  2. Pole sn kaka,maamuzi ulofanya niya kiume sn! Mwache aendelee na maisha yake kwa hizo tabia hakufai kaka.ww bado mdogo sn hadi ufike umri wake utapata life zaidi yake.ila hawa wanawake maarufu sio wa kuoa kabisa! U'r so HB kaka! Bado mdogo utampata unaemtaka tulia.pole Ezden..

    ReplyDelete
  3. mfupa uliomshinda fisi mbwa hauwezi.kwani dida anandoa ngapi mpaka leo.hiyo si bahati mbaya mda wake ulifika

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe ungemwacha aende wala asingepita kwenye mchujo kingereza cha kujifunza uzeeni tena nyumbani.

      Delete
  4. dah inaumiza sanah,ila yote maisha ndio tabia za wachache waliotangulia kuzitafuta wthr kwa njia sahh au tofaut,ila mwanangu ezel jifunze ucifny mistk once again,unaweza hata pekeyako kaza jembe

    ReplyDelete
  5. Hii tabia ya wanaume kuanza kulialia mbele ya vyombo vya habari kuhusu matatizo ya Ndoa zao imeanza lini?? Ilianza kwa Mbasha na sasa huyu naye. Hivi nyie wanaume vipi?? Mimi nilifikiri hiyo ni tabia ya wanawake sasa hata wanaume.....lools. Acheni ujinga nyie Wanaume. Shikeni majembe nendeni mkalime. Hizo tabia ziacheni kwa wanawake. By the way Wanawake ni wengi tu. Hamna sababu ya kukaa na kulilia kwenye vyombo vya habari. Mnatutia aibu wanaume wenzenu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Misenge utaijua tu! Ss nani anaelia lia? Huna bando la kutosha kuckiliza hiyo clip pita waachie wenye bando sio kucoment upuuz matako ww!?!

      Delete
    2. ni haki yake kutoa dukuduku lake la moyoni

      Delete
    3. Hii yote hawana pesa ndio maana mnaolewa kila kukicha, mwanaume mzima unalialia kwenye vyombo vya habari? WHAT A FOOL YOUR ARE LOOKING FOR EXECUSES

      Delete
    4. This comment has been removed by the author.

      Delete
  6. aaah eti ana bando .....kaka enelea na maisha yako una kazi rizika na unacopata achana na ilo gume gume ebo

    ReplyDelete
  7. msenge wewe unaeunga mkono mwanaume kutoa sili za ndani ,kama umeacha kaa kimya watu watajua tu.ni udhaifu kwa mwanaume lijari kuongea na wandishi au magenge ya watu mambo ya ndani wanawake wanakudhalau

    ReplyDelete
    Replies
    1. mficha malazi kifo humfichua bora kasema maana angekaa kimya kisha amtariki lawama zingekuwa zake na angepewa hila

      Delete
  8. Wewe anonymous 1:52 PM acha ujinga. Nenda kalime. Kama unafikiria biashara ya kukaaa na kulialia kuhusu wanawake inalipa basi kwa kweli wewe utakuwa ni msenge kabisa. Hufai kuitwa mwanaume. Hiyo biashara ya kulialia iacheni kwa wanawake. Mwanaume mzima unabakia oohhh yule sijui mwanamke wangu, oohh sijui nampenda sana.....kumanyoko zako wee.....nenda Shule na upate kazi ya maana uone kama wanawake hawatakulilia. Mna aibisha sana wanaume nyie. Sasa kama yule Mbasha oohh sijui nini. Na kumanyoko zake anabahati. Wangemwacha kwanza kama wiki moja hivi pale Keko wanaume wenzake wafire yale matako ndio angepata akili. Kazi kulia lia tu mxiuuuuuuuuu.....

    ReplyDelete
  9. Dida ni JLO wa bongo jamani.siku hizi super star wa bongo wanaiga kila kitu hadi kuolewa na kuachika.eti big brother kingereza issue kujitia aibu pamoja na nchi yetu.

    ReplyDelete
  10. big brother ya Kiswahili jamani mwaka huu au hamna habari?

    ReplyDelete
  11. Anonymous 1,52 na wasiwasi ni shoga.

    ReplyDelete
  12. dah jamani hv kuolewa na kuachika kila cku ni dili nn....me naona ata aibu huyo dida na big bro wapi na wapi jamani lol.....

    ReplyDelete
  13. Hee! dida sasa pumzika mwenzangu tafuta wa ku2 sugua kimya2 mwaya utakuwa una a leg na ndoa.ILa we nakuaminia sasa ivi utaanza dida wa nan cjui jaman usupa staa shida ungekuwa kitaa aka kimya2 sa2 uku blog umbea zote dida ye uwiiiiiiiii

    ReplyDelete
  14. sasa habari za huyo pimbi tumezichoka, tutoleeni picha zake, binafsi sioni maana yakuweka upuuzi huo hapo juu, watoe kabisa kahaba limeshindikana kila kona

    ReplyDelete
  15. Bro swala la kuoa sio kukurupuka epecially kama wote ni mastaa, nadhani haukufata ushaur wa watu wenye busara . ila hongera kwa kufanya maamuz hayo na kufunguka waz waz, umeonesha msimamo kama mwanaume, focus mbele forget abt the past

    ReplyDelete
  16. Bongonyoso Superstars sometimes wanajisahau,maisha yao halisi wanaishi kama wanaigiza.

    ReplyDelete
  17. Mwanaume kama binti lazima alie

    ReplyDelete
  18. Mwanaume kama binti lazima alie

    ReplyDelete
    Replies
    1. POLE SANA MDOGO TULIA UPATE ATAKAYE KUPENDA ACHA KUKURUPUKA HUYU NI KUKU WA KIENYEJI KILA JOGOO LINAPANDA

      Delete
  19. Hajazoe kula nyama tu lazima siku nyingine samaki na mboga za majani sasa wewe kila siku ale nyama tu haiwezekani, kuku wa kienyeji ukifuga ndani anataka atoke nje akutane na majogoo mengine. tulia hilo siyo tatizo watoto wa siku hizi wanaolewa kuondoa nuksi

    ReplyDelete
  20. pole sana kaka kwani katika maisha ya ndoa ukipata mke akasumbua anakuharibia ratiba zako usjai mungu ni mwema ujui kakuepusha na balaa gani?? utampata atakaye kuthamini endelea kuomba mungu akupe chaguo lako

    ReplyDelete

Top Post Ad